BAADA ya vuta nikuvute katika vyama vya siasa vinavyounda Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa), kuhusu kukubaliwa au kutokubaliwa kwa Waziri Mkuu Mstaafu, Edward Ngoyai Lowassa kujiunga na umoja huo ili kuongeza nguvu ya kisiasa, hatimaye mwanasiasa huyo maarufu nchini amekubaliwa na tayari amejiunga rasmi Ukawa akiwa mwanachama halisi wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), imefahamika.
Taarifa rasmi kutoka Ukawa na kwa msemaji wa Lowassa ambaye hakutaka jina lake litajwe, imeeleza kuwa uamuzi huo ulifikiwa baada ya majadiliano ya kina katika Mkutano Mkuu wa Ukawa uliofanyika mapema wiki hii huku ajenda kubwa ikiwa ni kumpokea Lowassa ili kuimarisha kambi ya upinzani ikiwa ni pamoja na kumsimamisha kama mgombea urais wa umoja huo.
BOFYA KUSOMA ZAIDI
BOFYA KUSOMA ZAIDI