



















Huu ni Mwenedelezo wa Mikutano ya Mh:Mwigulu Nchemba ya kuzungumza na Watanzania kuhusu Utekelezaji wa Ilani ya Chama cha Mapinduzi,Mchakato wa Katiba Mpya na Kujipanga kuelekea Uchaguzi wa Serikali za Mitaa na Uchaguzi Mkuu mwaka 2015,Wiki iliyopita Mh:Mwigulu Nchemba pia alizungumza na Wakazi wa Iringa Mjini viwanja vya Mwembetogwa kuhusiana na mambo tajwa hapo juu.
Mwigulu Nchemba ambaye ni Naibu Katibu Mkuu CCM_Bara ametumia sehemu Kubwa ya Hotuba yake kwa Wakazi wa Morogoro kuwaelimisha kuhusu Mchakato wa katiba Mpya ulipofikia na kile kinachozungumzwa na wanaojiita UKAWA kwenye Mikutano yao,Nchemba akizungumza kwa Msisitizo wa hali ya Juu amesema "UKAWA ni genge la Watu wachache waliodhamiria kusaka Madaraka kupitia idadi ya serikali,Wanazunguka Nchi Nzima kudanganya na Kuwagawa Watanzania kuhusu Serikali tatu,Haijawahi tokea wakatumia gharama kubwa kutekeleza miradi ya Maendeleo au Kuwaelimisha Watanzania kuhusu Kujiajiri,Wanatumia Fedha za Misaada na ruzuku kuzunguka Angani kuwahadaa Watanzania kuwa serikali tatu ni Suruhisho la Matatizo,Naomba kuuliza Serikali ya tatu Itajishughulisha na Afya,Elimu,Umeme,Barabara,Maji? Sasa tutatengenezaji Serikali inayokusanya kodi tu za Watanzania na kodi hiyo haitumiki kwenye mambo muhimu kwa Watanzania kama Afya,Elimu n.k?
Pia Watanzania Watambue wazi kuwa,Hakuna Serikali inayoendeshwa kwa gharama ndogo,Serikali ya tatu ikija hapa kodi itapanda na Uwezekano ni Mkubwa sehemu moja ya Muungano ikashindwa kuchangia Serikali hiyo ya tatu na hatimaye tukaigwa Nchi kwa Misingi ya Utanganyika na Uzanzibari kitu ambacho ni dhambi kubwa na haitatuacha salama.
Kuhusu Uchaguzi Ujao wa serikali za Mitaa na Uchaguzi Mkuu,Mh:Mwigulu Nchemba amewaomba Watanzania kuwa na Imani na chama cha Mapinduzi na Wandelee kuichagua CCM kama ilivyofanyika chaguzi za Nyuma na hata hizi za Karibuni,Kata 23,Majimbo ya Kalenga na Chalinze.Mkataba wa CCM na Watanzania ni Maendeleo na sio Kuzunguka na Helkopta kwa gharama kubwa kuitukana Serikali an Viongozi wake.
Mwisho Mh:Mwigulu Nchemba amesisitiza kuwa "Kitendo cha Wabunge wa Upinzani kutoka Nje ya Bunge liwe la Katiba au la Jamhuri ni kudhihirisha wazi kuwa hawafai hata kidogo kupewa Uongozi,huwezi kuwa na Kiongozi anayesusa kuwatumikia Wananchi wake,Wanasusia bajeti ya Nishati na Madini wanategemea Wananchiwao nani akawaombee Umeme Bungeni?Inasikitisha kuona Kambi ya Upinzani yenye Viongozi wabovu kama Tanzania,Viongozi wasiokuwa na VISION kuhusu Taifa lao,akili na mawazo yao wameelekeza kwenye Ubinafsi na Upotoshaji kwa Watanzania.Wanasahau kuwa Mwaka 2015 ni kesho kutwa na wengi wao ndio utakuwa Mwisho wao kuingia Bungeni wajiandae kuwa Wageni wetu tu.
Picha/Maelezo na Sanga Jr.