Quantcast
Channel: Blogu ya Wananchi
Viewing all 32622 articles
Browse latest View live

TAZAMA PICHA ZA MWANAMKE GUMZO ZAIDI NCHINI KENYA


MTANZANIA MUNA LOVE AONYESHA UREMBO WAKE KWA PICHA HIZI

MKE WA BILIONEA REGINAL MENGI JACQUELINE AACHIA PICHA HIZI

MREMBO PENDO KUTOKA KENYA AONYESHA PESA ZAKE HADHARANI

WAZIRI MKUU MAJALIWA ATEMBELEA HOSPITALI YA MKOA WA ARUSHA, AANZA ZIARA YA MONDULI

$
0
0
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akiwafariji wanawake waliolazwa kwenye wodi ya wazazi katika hospitali ya mkoa wa Arusha ya Mount Meru wakati alipotembelea wodi hiyo na kukuta wakiwa wamelala watatu kwenye kitanda kimoja Desemba 4, 2016.
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akielekea kwenye wodi ya wazazi katika hospitali ya mkoa wa Arusha ya Mount Meru wakati a;lipoitembelea Desemba 4, 2016. Kulia kwake ni Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mrisho Gambo.
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akisalimiana na viongozi wa wilaya ya Monduli baada ya kuwasili kwenye Ofisi ya Mkuu wa wilaya hiyo kuanza ziara ya siku moja ya kazi wilayani humo Desemba 4, 2016.

MWANZA NI HATARI,POLISI WAKAMATA SILAHA ZA KIVITA

$
0
0
MWANZA ni hatari. Ndivyo alivyosema Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mwanza, Ahmed Msangi, baada ya matukio mawili yaliyotokea usiku wa kuamkia jana, likiwamo la nyumba moja kukutwa silaha za kivita, za jadi na watoto 10 waliokuwa wakifundishwa mafunzo yanayoashiria kuwa ni ya kigaidi.Silaha zilizokutwa katika nyumba hiyo iliyopo Bugaka, Kata ya Kishili jijini Mwanza, ni bunduki aina ya AK 47, mabomu ya kurusha kwa mkono, bunduki aina ya Maker 4, risasi zaidi ya 150, majambia na visu.Akizungumza na MTANZANIA Jumapili katika mahojiano maalumu, Kamanda Msangi alisema kuwa aliongoza vijana wake kufika katika nyumba hiyo baada ya kupata taarifa kutoka kwa baadhi ya watuhumiwa wanaowashikilia kwa matukio mbalimbali, kwamba wafadhili wao wapo Kishili na Buhongwa.
Msangi alisema kutokana na taarifa hizo, aliunda vikosi viwili kufanya operesheni maalumu usiku wa kuamkia jana, kimoja kilikwenda eneo la msitu wa Deo uliopo Buhongwa na kingine Kishili.
Akizungumzia kikosi cha Kishili alichokiongoza, alisema walipofika katika nyumba hiyo waliizingira na watu waliokuwamo ndani wakaanza purukushani za kutaka kujihami ndipo askari walilazimika kufyatua risasi moja kuwatuliza.
Kamanda Msangi alisema wakati wanatafuta namna ya kuingia ndani ya nyumba hiyo iliyo na uzio, kijana mmoja alifanikiwa kuruka ukuta kwa upande wa nyuma na kutoroka, lakini wakafanikiwa kuwadhibiti wenzake zaidi ya 15.
“Baada ya kuwadhibiti na kuingia ndani, tulifanya ukaguzi na kufanikiwa kupata mabomu ya kurusha kwa mkono yaliyokuwa yameandaliwa kwa matumizi, bunduki za kivita aina ya AK 47, magazine tano na kila moja ikiwa na risasi 30, majambia, bunduki ndogo aina ya Maker 4, visu na gari moja ambayo inawezekana ndiyo wanayotumia kufanya doria zao kabla ya kufanya matukio.
“Tulipoingia tumewakuta watoto wadogo 10 waliokuwa wakifundishwa mafunzo maalumu ya namna ya kutumia silaha walizokuwa nazo na namna ya kujilinda na adui, pia kulikuwa na wanaume wanne wakubwa na wanawake wawili ambao inaelezwa ndio watoaji mafunzo kwa watoto hao.
“Katika mahojiano ya awali, tumeelezwa kwamba watu hao wana vikosi katika mikoa mbalimbali ya Kanda ya Ziwa, ikiwamo Tabora, Mwanza na Kigoma,” alisema.
Kamanda Msangi alisema wakati wanapambana na watuhumiwa hao, wananchi walijikusanya eneo hilo, wakiwa na nia ya kutaka kuwaua watuhumiwa hao, lakini askari walisimama imara na kufanikiwa kuondoka nao wakiwa hai.

Alisema baada ya kuondoka na watuhumiwa hao, baadaye alipata taarifa kwamba wananchi waliamua kuteketeza nyumba hiyo kwa moto alfajiri ya jana.

WAWILI WAUAWA

Akizungumzia kikosi cha pili kilichokwenda msitu wa Deo, alisema kiliambatana na vijana wanne ambao baadhi yao ni waendesha bodaboda, waliokuwa wakishikiliwa kwa matukio ya hivi karibuni.

Alisema walipofika katika msitu huo, walionyesha silaha zilipo na katika ukaguzi walifanikiwa kupata bunduki moja aina ya SMG, magazine mbili huku moja ikiwa na risasi 15 na nyingine 30, pia walikamata bastola moja.

“Wakati askari hao wakifanya upekuzi katika msitu huo, ghafla watuhumiwa hao walianza purukushani ya kutaka kutoroka, ndipo askari waliwafyatulia risasi na kuwaua wawili.

“Tunaendelea kuwahoji watuhumiwa ili kupata mtandao wote, lakini hapa Mwanza ni hatari, kibaya zaidi vijana hawa wa bodaboda wanajihusisha na vitendo hivi, tunaomba wananchi kuwa makini na kundi hili,” alisema.

BREAKING NEWS : MCHEZAJI WA MBAO FC AFARIKI BAADA YA KUGONGANA NA MCHEZAJI WA MWADUI FC LEO

$
0
0
Mshambuliaji wa timu ya vijana ya Mbao FC U-20 Ismail Mrisho Khalfan anayevalia jezi nambari 4 amefariki Dunia jioni hii baada ya kuanguka uwanjani Kaitaba wakati wa mtanange wao dhidi ya timu ya vijana wa Mwadui FC ikiwa ni mechi ya mwisho ya kumaliza duru la kwanza la ligi ya Vijana.
Ismail Khalfan amefariki baada ya kufikishwa Hospitali ya Serikali ya mjini Bukoba.

Ismail Khalfan kabla ya kufikiwa na umauti aliweza kuifungia timu yake bao la kwanza na bao la pili lilifungwa kwa mkwaju wa Penati hivyo mtanange kumalizika kwa 2-0.

Kabla ya kuanguka Ismail aligongana na beki wa Mwadui FC na baadae akiwa peke yake alianguka chini lakini akainuka halafu akaanguka tena na kutokana na ukosefu wa huduma ya kwanza na gari la wagonjwa katika Uwanja wa Kaitaba kulipelekea marehemu kupandishwa kwenye gari la zima moto na kupelekwa hospital ambapo mauti yalimkuta.

PICHA ZA MASOGANGE ZAWA KIVUTIO INSTAGRAM


MAJALIWA AITEMBELEA FAMILIA YA MAREHEMU SOKOINE MONDULI JUU

$
0
0
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akisalimiana na Napono Sokoine (wapili kulia) na Nekiteto Sokoine (kulia) ambao ni wajane wa aliyekuwa Waziri Mkuu, Marehemu Edward Sokoine wakati aipokwenda nyumbani kwa marehemu, Monduli Juu kuisalimia familia akiwa katika ziara ya wilaya ya Monduli leo Desemba 4, 2016.
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akiweka shada la maua kwenye kaburi la aliekuwa Waziri Mkuu, Edward Sokoine wakati alipokwenda nyumbani kwa marehemu, Monduli Juu akiwa katika ziara ya wilaya ya Monduli leo
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akizungumza wakati alipokwenda nyumbani kwa aliyekuwa Waziri Mkuu, Edward Sokoine, Monduli Juu kuisalimia familia akiwa aktika ziara ya wilaya ya Monduli Desemba 4, 20, 16. Kushoto kwake wajane wa marehemu, Napono Sokoine (wpili kulia) na kulia ni Nekiteto Sokoine . Kulia kwake ni Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Mrisho Gambo.
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akizungumza wakati alipokwenda nyumbani kwa aliyekuwa Waziri Mkuu, Edward Sokoine, Monduli Juu kuisalimia familia akiwa aktika ziara ya wilaya ya Monduli Desemba 4, 20, 16. Kushoto kwake wajane wa marehemu, Napono Sokoine (wpili kulia) na kulia ni Nekiteto Sokoine . Kulia kwake ni Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Mrisho Gambo.(Picha na Ofisi ya Wziri Mkuu)

SUPER STAR SHILOLE TRUMP NI KIBOKO,AAMUA KUANIKA MAMBO LIVE

THE MAGAZETI YA BONGO LEO MONDAY/JUMATATU 5/12/2016 LIVE

MZEE WA UPAKO AWACHIMBA MKWARA KWA WANAODAI ANATUMIA ULABU

$
0
0
mzee-wa-upako3

Baada ya hivi karibuni kuenea habari kuwa mchungaji wa kanisa la Maombezi, Anthony Lusekelo amemfanyia fujo jirani yake hivyo kushikiliwa na polisi na kwamba alionekana akiwa amelewa pombe, ameibuka na kuwaonya wale wanaozusha habari za uongo.


Akiwahubiria waumini wake Jumapili hii, Mchungaji huyo alisema, “Wiki iliyopita nilikuwa wizara ya mambo ya ndani, baadhi ya maofisa wakaniona, wewe mzee wa upako, wewe mzee wa upako, askari mmoja akaniuliza unachukua sadaka unaenda kunywa pombe. Nikawauliza hiyo pombe nilikunywa wapi, halafu pombe zipo nyingi, taja ni pombe gani, ukienda mbali zaidi ungeuliza nililewa nini, maana hata upako wa roho mtakatifu ni ulevi.”
Mchungaji huyo aliongeza kuwa hakuna binadamu atakayeweza kumwangusha kwa kipawa na karama aliyopewa na Mungu.
BY: EMMY MWAIPOPO
CHANZO: MWANANCHI

THE KING OF ALL BONGO SOCIAL MEDIA NETWORK LE MUTUZ HANGING OUT WITH WEMA SEPETU LIVE!!

$
0
0

The King Of All Bongo Social Media Network Le Mutuz Nation, hanging out with Super Star Wema Sepetu and Super Bilioneaz Lady Nana Billy at the Tasty Bekary Mikochen, the new Joint Caffee inayokimbiza sana hapa mjini sasa hivi live!!








PICHA ZA KWANZA ZA TIMU YA SOKA YA WABUNGE WA TANZANIA WAKIWA NCHINI KENYA LIVE!!

$
0
0
Timu ya Wabunge wa Tanzania iliyokwenda Kenya kwa ajili ya kupambana na Timu ya Wabunge wa Kenya ikiwa matayarishoni Mjini Mombasa live!!











TAARIFA YA VIKAO VYA KAMATI KUU NA HALMASHAURI KUU.


RAIS DKT. MAGUFULI AKUTANA NA MKURUGENZI WA MAUZO WA KAMPUNI YA NDEGE YA BOEING

$
0
0

 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akisalimiana na Mkurugenzi wa mauzo wa kampuni ya Ndege ya Boeing Jim Deboo aliyefika Ikulu kwa ajili ya mazungumzo pamoja na ujumbe wake.
  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akitazama kitabu cha  picha ya ndege aina ya Boeing 787-8 Dream liner wakati alipokuwa akisikiliza maelezo yake kutoka kwa Mkurugenzi wa mauzo wa kampuni ya Ndege ya Boeing Jim Deboo. Ndege hiyo itakuwa na uwezo wa kubeba abiria 262 na itakuwa na uwezo wa kuruka kutoka nchini Marekani hadi Tanzania bila kutua mahali popote.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akimshukuru Mkurugenzi wa mauzo wa Kampuni ya Ndege ya Boeing Jim Deboo mara baada ya kumaliza mazungumzo yao Ikulu jijini Dar es Salaam. Wa kwanza kushoto ni Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha Doto James na anayefuatia ni Katibu Mkuu wa Sekta ya Uchukuzi Dkt. Leonard Chamuriho.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza kuhusiana na ununuzi wa ndege hiyo mpya aina ya Boeing 787-8 Dream liner mara baada ya kumaliza mazungumzo na Mkurugenzi wa mauzo wa Kampuni ya Ndege ya Boeing Jim Deboo Ikulu jijini Dar es Salaam.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akisalimiana na Balozi wa Cuba anayemaliza muda wake nchini George Luis Lopez Tormo aliyefika Ikulu jijini Dar es Salaam.
  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza na Balozi wa Cuba anayemaliza muda wake hapa nchini George Luis Lopez Tormo aliyefika Ikulu jijini Dar es Salaam kwa ajili ya kuaga.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiagana na Balozi wa Cuba anayemaliza muda wake hapa nchini George Luis Lopez Tormo Ikulu jijini Dar es Salaam.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akisalimiana na Mwakilishi Mkazi wa Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB) Dkt. Tonia Kandiero aliyefika Ikulu kwa ajili ya mazungumzo. Dkt. Tonia ameteuliwa kuwa Mkurugenzi Mkuu wa Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB) katika Ukanda wa Kusini Mwa Afrika katika Ofisi zake zilizopo Afrika ya Kusini
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiagana na  Mwakilishi Mkazi wa Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB) Dkt. Tonia Kandiero ambaye alifika Ikulu kwa ajili ya mazungumzo na kuagana na Mhe. Rais Dkt. Magufuli. Dkt. Tonia ameteuliwa kuwa Mkurugenzi Mkuu wa Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB) katika Ukanda wa Kusini Mwa Afrika katika Ofisi zake zilizopo Afrika ya Kusini
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akijadiliana jambo na Mwakilishi Mkazi wa Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB) Dkt. Tonia Kandiero ambaye alifika Ikulu kwa ajili ya mazungumzo.Dkt. Tonia Kandiero ameteuliwakuwa  Mkurugenzi Mkuu wa Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB) katika Ukanda wa Kusini Mwa Afrika katika Ofisi zake zilizopo Afrika ya Kusini PICHA NA IKULU 

LOO! NISHA SI KWA DHARAU HIZI AMEFUNGUKA HAYA KUHUSU UJAUZITO WAKE NA BARAKA THE PRINCE

$
0
0

Muigizaji wa filamu Salma Jabu ‘Nisha’ amemfungukia msanii machachari wa muziki wa bongo flavour Baracka Da Prince  kuhusu madai ya mimba yake. 

Nisha amedai kuwa endapo ujauzito wake ungekuwa wa Baraka The Prince kama inavyosemwa na wengi basi ungetoka wenyewe mapema kwa kuwa muimbaji huyo ni miongoni mwa wanaume asiowapenda duniani.

Akizungumza katika kipindi cha FNL cha EATV, Nisha amesema siri ya mimba yake anayo moyoni na hana haja ya kumtaja mwanaume aliyempatia mimba hiyo.
“Kama hii mimba ingekuwa ya Baraka, ingetoka yenyewe, wala isingesubiri” Alisema Nisha.
Kuhusu muhusika wa ujauzito huo, Nisha ameendelea kufanya siri na kuapa kutomtaja kabisa hata siku moja licha ya watu kutaja baadhi ya majina ya watu maarufu ambao amekanusha kuwa siyo wahusika.
Katika hatua nyingine Nisha aliweka wazi kuwa anatarajia kujifungua mtoto wa kiume, licha ya kuwa bado hajamtafutia jina.

Kuhusu mazingira aliyopata ujauzito huo, Nisha ambaye alijikuta akimwaga chozi studio, alisema mwanaume aliyempa ujauzito alimlazimisha kufanya naye mapenzi, na kwamba ahaikuwa ridhaa yake na ndipo ikatokea hivyo.

WIKI YA KUTOA HUDUMA KWA WANANCHI KATIKA KUADHIMISHA SIKU YA MAADILI NA HAKI ZA BINADAMU YAZINDULIWA RASMI JIJINI DAR ES SALAAM.

$
0
0

 Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais - Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe. Angellah J. Kairuki (Mb) akitoa neno la utangulizi wakati wa uzinduzi wa Wiki ya kutoa huduma kwa wananchi katika kuadhimisha Siku ya Maadili na Haki za Binadamu inayofanyika katika viwanja vya Mnazi Mmoja, Dar es Salaam.
 Waziri wa Katiba na Sheria, Mhe. Dkt. Harrison Mwakyembe (Mb) akizindua rasmi Wiki ya kutoa huduma kwa wananchi katika kuadhimisha Siku ya Maadili na Haki za Binadamu inayofanyika katika viwanja vya Mnazi Mmoja, Dar es Salaam.
Baadhi ya watumishi wa taasisi zinazosimamia maadili, uwajibikaji, utawala bora, haki za binadamu na mapambano dhidi ya rushwa nchini wakimsikiliza Waziri wa Katiba na Sheria, Mhe. Dkt. Harrison Mwakyembe (Mb) alipokuwa akizindua rasmi Wiki ya kutoa huduma kwa wananchi katika kuadhimisha Siku ya Maadili na Haki za Binadamu inayofanyika katika viwanja vya Mnazi Mmoja, Dar es Salaam.
  Waziri wa Katiba na Sheria, Mhe. Dkt. Harrison Mwakyembe (Mb) na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe. Angellah J. Kairuki (Mb) wapata maelezo kutoka kwa mmoja wa watumishi wa Ofisi ya Rais-Utumishi kuhusu kazi  zinazofanywa na Idara ya Uendezaji Maadili wakati wa Wiki ya kutoa huduma kwa wananchi katika kuadhimisha Siku ya Maadili na Haki za Binadamu inayofanyika katika viwanja vya Mnazi Mmoja, Dar es Salaam.
Waziri wa Katiba na Sheria, Mhe. Dkt. Harrison Mwakyembe (Mb) na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe. Angellah J. Kairuki (Mb) wakishangilia baada ya kukata utepe kuzindua rasmi Wiki ya kutoa huduma kwa wananchi katika kuadhimisha Siku ya Maadili na Haki za Binadamu inayofanyika katika viwanja vya Mnazi Mmoja, Dar es Salaam.

GUCCI MANE AWEKA WAZI LINI ATAFUNGA NDOA NA MCHUMBA WAKE

$
0
0
Miezi miwili baada ya kutoka jela na kuachia ngoma mpya mtaani, Gucci Mane ameweza kupata nafasi ya kumvalisha mpenzi wake Keyshia Ka’oir pete ya uchumba.

laflare1017-20161205-0001
Gucci Mane & Keyshia Ka’Oir
Na sasa good news nikwamba, Gucci Mane na Mpenzi wake wametangaza rasmi watafunga ndoa October 17, 2017.
Siku hio ni muhimu kwa Gucci, ambayo aliwahi kuimba kwenye 1017 Brick Squad na hata jina analotumia kwenye mtando wa twitter ni @Gucci1017.
Namba hii ni namba ya nyumba ya babu yake
kama alivyowahi kuimba kwenye wimbo wake
“Decapitated” kwenye album yake ya mwaka 2013 Diary of a Trap God.

MREMBO TINY AMCHANA MUME WAKE

$
0
0
Baada ya kusambaa kwa video inayo muonesha mke wa rapper T.I, Tiny akicheza muziki na Floyd Mayweather, kulizuka tetesi za usaliti katika ndoa yao.

thetinyharris-20161205-0002
T.I & Tiny Harris
Mbaya zaidi ni kuwa T.I na Mayweather wana bifu ya muda mrefu na walishawahi kupigana. Video hiyo ilimfanya rapper huyo amchane kwa mafumbo mke wake na kuashiria kuwa hajapendezwa.
Na sasa mke wake Tiny ametumia mtandao wa Facebook kumjibu mume wake. Anadai kuwa kwa miaka mingi ni yeye ndiye amekuwa akiumizwa na anamshangaa kwa kukasirishwa na video hiyo inayo muonesha akicheza muziki na rafiki yake.
“When a woman’s fed up… For years i’ve been the one getting hurt, but now that a lil video done surfaced with me having a friendly dance , he’s mad?? Why? Yes, he’s my husband but damn can I not have a male friend?! Tip can’t be the only male friend I associate myself with just like I know I ain’t the only Female he associate hisself with so… It is what it is,” ameandika.
Viewing all 32622 articles
Browse latest View live


<script src="https://jsc.adskeeper.com/r/s/rssing.com.1596347.js" async> </script>