Quantcast
Channel: Blogu ya Wananchi
Viewing all 32622 articles
Browse latest View live

KIZUNGUMKUTI CHA BVR DAR ES SALAAM

$
0
0
Kina mama na watoto wakiwa wamelala wakisubiri kujiandikisha kwenye daftari la kudumu la wapigakura katika Kituo cha Ulongoni, Gongo la Mboto, Dar es Salaam jana. Picha na Venance Nestory

Wakati uandikishaji wa wananchi katika Daftari la Kudumu la Wapigakura, ukiingia siku ya tatu leo, kasoro lukuki zimeendelea kugubika mchakato huo huku katika baadhi ya vituo wananchi wakizichapa wakigombania kuingia chumba cha kujiandikisha.
Tukio la kutwangana makonde lilitokea katika Kituo cha Shule ya Mwangaza, Gongo la Mboto saa 2.15 asubuhi wakati uandikishaji ulipokuwa ukianza.
Mashuhuda wa tukio hilo walisema: “Polisi unaowaona wamefika muda si mrefu, wala hawakuwepo hapa tangu asubuhi... ninadhani walipewa taarifa baada ya watu kuanza fujo wakigombania kuingia ndani kujiandikisha,” alisema Magreth John na kuongeza:(P.T)
“Watu wamepigana kwa sababu wanasema kuna wenzao ambao majina yao hayakuandikwa jana (juzi) halafu wamefika asubuhi wakaanza kuitwa ndani kujiandikisha. Hapo ndipo mzozo ulipoanzisha na ngumi zikafumuka.”
Msimamizi wa kituo hicho, Ramadhani Mshindo alisema mzozo huo ulitokea kwa sababu ya wananchi hao hawakuelewa utaratibu.
“Jana (juzi) jioni wakati tunafunga zoezi hili saa 12.00 jioni kuna watu wengi walikuwa kwenye foleni ambao hawakuandikishwa, kwa hiyo tuliwaandika majina ili leo (jana) wakifika hapa watangulie kuandikishwa kabla ya wengine. Sasa tulivyofika na kuanza kuita majina yao ili waingie kujiandikisha ndipo watu wakaanza fujo na kupigana ikabidi tupige simu polisi ili waje kutuliza ghasia,” alisema Mshindo.
Katika Kituo cha Shule ya Msingi Jica, Tabata wananchi walilalamikia suala la muda kwani waandikishaji walichelewa na hadi saa 4.30 asubuhi, asilimia kubwa ya watu hawakuwa wamepata huduma. “Nimefika hapa saa 12.00 asubuhi lakini hadi sasa sioni dalili ya kuandikishwa leo... Wametuambia wanaanza kuandikisha wale waliobaki jana kwa sababu majina yao yaliandikwa kwa hiyo sisi wa leo tunasubiri kwanza,” alisema Maria Saleh.
Maria alisema uandikishaji unakwenda taratibu kutoka na mashine kugoma mara kwa mara.
Malalamiko kama hayo yalitolewa na wananchi waliokuwa wamefika kujiandikisha katika Kituo cha Shule ya Msingi, Ulongoni, Gongo la Mboto na waandishi wetu walishuhudia watu wengi wakiwa kwenye misururu, wengine wakiwa wamelala pembeni ya kituo hicho baada ya kuchoka kusimama muda mrefu.
Hata hivyo, kwenye kituo hicho, wananchi walijiwekea utaratibu kwamba kila mtu anayefika anaandika namba kwenye daftari na kupewa kikaratasi kidogo chenye namba hiyo ndipo anapanga foleni.
Utaratibu ambao ulisaidia kupunguza usumbufu na kuondoa vuta ni kuvute wakati wa kuingia kwenye chumba cha kujiandikisha.
Lakini licha ya kujiweka utaratibu huo, Ibrahim Kitumbi alisema changamoto ya muda na vifaa ilikuwa palepale.
“Hivi tunavyozungumza watu waliyopewa namba wamefika 2,145. Hawa wameandika majina tu na kupewa namba. Waliojiandikisha tangu jana hawafiki hata 200. Sasa kwa siku nane zilizobaki kweli tunaweza kumaliza kuandikishwa! Huku si kutunyima haki?” alihoji.
Wakati wananchi wakitoa malalamiko hayo, Ofisa Mtendaji wa Mtaa wa Ulongoni, Majura Mtalemwa alisema zoezi la uandikishaji linakwenda vizuri tofauti na wananchi wanavyolilalamikia.
Mkazi wa Temeke, Steven Almasi aliyefika kujiandikisha katika Kituo cha Magogoni, Yombo alisema mwaka huu wa uchaguzi kuna uwezekano mkubwa wa baadhi ya wananchi kutoshiriki uchaguzi.
Mtendaji wa mtaa huo, Zeddy Zeddy alikiri kuwapo baadhi changamoto kwenye kituo chake ikiwamo uchache wa mashine za kuandikisha.
“Mwitiko wa watu umekuwa mkubwa tofauti na matarajio yetu kwa hiyo kama mashine zikiongezwa kwenye baadhi ya vituo, itasaidia kuondoa msongamano na kazi kukamilika kwa wakati,” alisema Zeddy.
“Kama Tume ingeongeza mashine, mambo yangekwenda vizuri zaidi lakini kinachoendelea ni ngumu kusema kuwa watu wote wataandikishwa kama ilivyopangwa,” alisema mtaalamu wa BVR aliyekuwapo Kituo cha Shule ya Msingi Kibangu, Ubungo, Suleiman Mahmoud.
Katika kituo cha Kontena – Tanesco, Kinondoni ni mashine moja tu iliyokuwa ikifanya kazi kati ya tatu kutokana na kuharibika licha ya idadi ya watu kuwa wachache.
“Mashine moja ilikuwa haifanyi kazi hadi saa tatu asubuhi, wameleta nyingine lakini nayo kamera inasumbua. Hii yangu printa haifanyi kazi hivyo ipo moja tu. Tumewapigia IT (mafundi wa Teknolojia ya Mawasiliano) wamesema wanakuja lakini wengi wanatembea kwa miguu wanachelewa kufika,” alisema mwendeshaji mashine ya BVR kituoni hapo, Max Phillipo.
Mkazi wa Mwananyamala, Hemed Shefaya alisema alifika kituoni tangu saa 10 alfajiri akiwa na wenzake watatu lakini kilifunguliwa saa 2.30 asubuhi.
“Mashine hizi zinaharibika mara kwa mara, kwa sasa wamezitengeneza lakini mikono ya wasimamizi ni mizito sana. Tulikuja jana na kupatiwa namba lakini hatukufanikiwa kuandikishwa... fikiria mimi namba 18 ya jana nimekuja saa 12 asubuhi lakini bado hadi sasa (saa 5.43) sijaandikishwa,” alisema Ramadhani Mkombozi aliyekuwa katika Kituo cha Shule ya Msingi Kisiwani, Mwananyamala.
Ofisa Uchaguzi wa Manispaa ya Kinondoni, Valence Urassa alisema tatizo la kuharibika kwa BVR lilikuwa likifanyiwa kazi na mafundi wa NEC na Manispaa na kwamba maeneo yenye wakazi wengi yalikuwa yakiongezwa mashine kufikia mbili kila kituo.
Kuhusu kuchelewesha kufungua vituo, alisema kituo chochote hakitafunguliwa 2.00 asubuhi iwapo waandikishaji hawatakuwa wamekamilisha maandalizi ya vifaa na kuandikisha kwani kuwahisha kutaleta matatizo.
Baadhi ya wasimamizi wametoa wito kwa NEC kuongeza vifaa pamoja na wataalamu ili kazi hiyo ikamilike kwa wakati.
Msimamizi wa Kituo cha Chuo cha Usafirishaji (NIT), Kelvin Donald alisema mashine alizonazo zinasumbua tangu juzi na hata baada ya kutoa taarifa na kubadilishiwa bado tatizo hilo linaendelea.
“Kwa wastani wanajitokeza watu 1,200 kila siku na hapa tuna mashine tano tu, moja haifanyi kazi,” alisema Donald.
Mwenyekiti wa Serikali ya Mtaa wa Mbezi Luis, Omari Mshauri alisema baada ya umeme kuwa kikwazo, juzi msamaria mmoja alijitolea jenereta huku wengine wakichangia mafuta kuendelea na kazi.
NEC yafafanua
Mkurugenzi wa Uchaguzi wa NEC, Julius Malaba alisema wakazi wote wa jiji hili waliojitokeza wataandikishwa hata baada ya siku zilizopangwa kumalizika hivyo hawatakiwi kuwa na hofu.
“Hakuna mtu aliyejitokeza kuandikishwa halafu akaachwa... tutaandikisha mpaka wote waliojitokeza siku ya mwisho watakapokamilika.
“Mpaka sasa tuna mashine takriban 3,500 na nyingine zinaendelea kuingia kutoka mikoa ambayo tumeshakamilisha kuandikisha. Hizi zote zitaletwa kuongeza nguvu ya uandikishaji katika maeneo yenye wakazi wengi na kumaliza haraka,” alisema Malaba.
Kawe kujiandikisha upya
Malaba alieleza kuwa wakazi wa Jimbo la Kawe ambao walijiandikisha awali katika uandikishaji wa majaribio, watatakiwa kujiandikisha upya ili wapate vitambulisho vya sasa.
Hata hivyo, hakutaja sababu za kurudia na kuahidi kufafanua zaidi leo.
RC atoa maagizo
Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Said Meck Sadik amewataka wakurugenzi wote wa Manispaa za Dar es Salaam kutoka maofisini na kwenda kusimamia kwa karibu uandikishaji huo na kutatua matatizo yanayoripotiwa na wananchi kila wakati.
Alisema amepokea malalamiko mengi kutoka kwa wananchi, mojawapo likiwa waandikishaji kuchelewa kufika vituoni, kuwahi kuondoka kabla ya muda na mashine kugoma.
“Tutachukua hatua kali kwa ofisa mwandikishaji yeyote atakayekiuka taratibu na kukwamisha uandikishaji... tunafahamu uandikishaji unakabiliwa na changamoto nyingi, lakini nimepata taarifa kuwa waandikishaji pia wanahujumu uandikishaji bila sababu za msingi,” alisema Sadik.

PICHA MBILI ZA ZARI BIG BOSS LADY UWONE ALIVYOKUWA MLITO UTADHANI SIO MAMA WA WATOTO WA 3

DAVIDO KUIMBA WIMBO NA ALI KIBA

$
0
0
Staa wa muziki kutoka Nigeria, Davido.
STAA wa muziki kutoka Nigeria, Davido ameweka wazi kuwa ana mpango wa kuimba wimbo kwa kushirikiana na Ali Kiba na mchakato unaendelea kimyakimya.(P.T)
Ali Kiba.
Davido ambaye jina lake lilipata umaarufu nchini kutokana na kushirikiana na Diamond katika Wimbo wa Number One Remix, aliweka wazi hayo wakati akipita kwenye ‘red carpet’ kwenye usiku wa Tuzo za MTV Mama, wikiendi iliyopita.

“Tanzania ni nyumbani kwangu baada ya Nigeria, napapenda tangu siku ya kwanza nilipofika, nitafanya kazi pia na Ali Kiba, naamini itakuwa bomba, watu wasubiri tu,” alisema Davido bila kufafanua zaidi.

TETESI ZA LOWASSA KUHAMA CHAMA LACHUKUA SURA MPYA ,MAMA REGINA AINGILIA KATI

$
0
0
Shinikizo dhidi ya Waziri Mkuu wa zamani, Edward Lowassa, la kumtaka akihame Chama Cha Mapinduzi (CCM) linazidi kuongezeka na katika timu yake ya ndani ni watu wawili tu wanaonekana kumtaka abakie ndani ya chama hicho. Habari za ndani ya vikao vya kujadili hatua za kuchukuliwa na Lowassa baada ya jina lake kukatwa kwenye mchakato wa kugombea urais kupitia CCM, zinasema kuwa wandani wake wanaamini kuwa hana atakachopata kama ataendelea kubaki kwenye chama hicho tawala.
"Kaka sikiliza, inavyoelekea shinikizo dhidi ya Lowassa ni kubwa sana. Watu wake wa ndani wanataka aondoke CCM. Wanaona kama amedhalilishwa mno,"kilisema chanzo chetu ndani ya vikao hivyo.  






THE MAGAZETI YA BONGO LEO SATURDAY/JUMAMOSI 25/7/2015 LIVE!!

KUTANA NA MABINTI AMBAO USTAA UMEWASHINDA BONGO MUVI!

$
0
0
Skaina Ally Skaina AllyWapo mabinti ambao waliingia kwenye fani ya uigizaji kwa mbwembwe, wakawika sana kwenye vyombo vya habari na kuunyemelea ustaa lakini ghafla wakayeyuka.Walipoibukia kwenye fani walionekana watakuwa tishio na kuwafunika wale wakongwe waliokuwa wakionekana wao ndiyo wao. Sasa hivi hawajulikani wako wapi na wanafanya nini. Huyu alikuwa tishio sana miaka ya nyuma. Umbo lake tata, uzuri wake vilimbeba, akawavutia baadhi ya wanamuziki ambao walimfanya kuwa Video Queen kwenye nyimbo zao kama vile Bob Junior
aliyemtumia kwenye ‘kichupa’ chake cha Wimbo wa Kimbiji.
Aliigiza kwenye filamu mbalimbali kupitia Kampuni ya RJ. Hata hivyo, baadaye aliolewa kisha akaachika, mara akabeba ujauzito uliodaiwa ni wa mwanamuziki Nay wa Mitego. Baada ya kujifungua akawa kimya, mwanaye ni mkubwa lakini haijulikani sasa anafanya nini.

Zamda Salim
Huyu naye aliibuka miaka 2010 kwenye soko la filamu. Ana umbo zuri lililomfanya atumike kwenye filamu kadhaa.
Naye alionekana kuja kuwafunika mastaa lakini cha kushangaza akaanza kufifia na mpaka sasa hata wewe msomaji unayefuatilia masuala ya burudani ukiulizwa yuko wapi na anafanya nini huwezi kuwa na jibu.Mara ya mwisho zilivuja picha akiwa amevaa shela, watu wakasema ameolewa lakini wengine wakadai ni filamu.

Zamda Salim Ester Flaviana
Huyu ni mmoja wa maandagraundi walioibuka kwa kasi ya ajabu. Aling’ara kwenye magazeti, akaonekana kwenye filamu mbalimbali lakini naye mara ya mwisho zilivuja picha zake za utupu na mpaka leo hii haijulikani kajichimbia wapi.

Diana Kimaro
Diana Kimaro ni binti f’lani mcharuko. Mcharuko wake umeonekana kwenye filamu mbalimbali alizocheza kama vile Family Disaster. Aling’ara sana alipokuwa akiigiza kwenye filamu kama Pacha wa Elizabeth Michael ‘Lulu’.
Mara ya mwisho alikuwa akisoma Moshi kisha baadaye akaonekana kwenye filamu ya Msuto Daily na Kigodoro lakini hawiki kama anavyowika shoga yake Lulu.

Rehema Fabian
Aliibukia kwenye Shindano la Miss Kiswahili 2008, akapaa zaidi pale alipokuwa akitoka kwenye magazeti na skendo tofauti huku akionekana kwenye filamu mbalimbali.Mara ya mwisho alikimbilia nchini China ambapo alidai kuchumbiwa na mtoto wa kigogo wa Nigeria. Juzikati ilisemekana ni mjamzito, amekaa kimya haijajulikana anafanya nini.

Neema Chande
Huyu alitokea kwenye umiss, alivuma sana alipojiingiza kwenye masuala ya filamu na kufikia hatua ya kutoa filamu yake aliyoipa jina la Time Goes Around. Alipamba kurasa mbalimbali za magazeti kwa habari zake tofauti.
Staa huyu kwa sasa yupo nchini India, anaonekana kwenye mitandao tu ya kijamii, haijulikani anafanya nini huko lakini kwenye anga za mastaa amepotea kabisa.

Pendo wa Maisha Plus
Jina lake kamili ni Upendo Mushi. Staa huyu aliibukia kwenye Shindano la Maisha Plus. Baada ya hapo alicheza kwenye filamu mbalimbali. Kuna kipindi ilidaiwa kutoka na marehemu Kanumba na Diamond Platnumz.
Lakini naye sasa hivi haijulikani anafanya nini. Wapo wanaosema anaigiza lakini habari zake zimekuwa ngumu kuzipata tofauti na ilivyokuwa zamani ambapo alikuwa hakauki kwenye vyombo vya habari.

Amisuu Malick
Huyu naye alipamba kurasa za magazeti baada ya kuibukia kwenye umiss. Wapo wanaodai alichumbiwa ndiyo sababu ya kuwa kimya.Marafiki zake wa karibu wanasema kuwa ameamua kutulia na kufanya mambo yake ambayo si lazima yaanikwe hadharani.

Sharzy Sadry
Huyu naye ni staa ambaye alitoka na marehemu Steven Kanumba kwenye filamu ya ‘The Shock’. Alionekana kuwashtua mastaa wa Bongo kwani filamu hiyo aliicheza kwa umahiri.Wapo waliosema kuwa Kanumba alimchukua ili kuziba pengo la Wema kwani kwa wakati huo Wema na Kanumba walikuwa wameachana.

Halima Madiwa
Aliibukia kwenye uigizaji wa filamu. Waliomchezesha kwenye filamu waliamini kuwa angekuja kuwa tishio. Akawa hakauki kwenye magazeti lakini naye cha ajabu kapotea.

BALAA LA WAJAWAZITO KUPENDA CHIPSI KUKU!

$
0
0
Mtoto aliyezaliwa akiwa na kichwa kikubwa. Dokta Agricore aliyasema hayo alipokutana na MC maarufu jijini Dar, Joyce Amina Mwakipunda ‘Mc Jojo’ na Mtangazaji wa Kipindi cha Tashtiti Zetu cha Redio Uhuru, Nuru Issa, walipofika hospitalini hapo kutoa misaada mbalimbali kama vile pampasi, mafuta, poda, maji ya kunywa, juisi ikiwa ni sehemu ya kuadhimisha siku yao ya kuzaliwa.

Ugonjwa unaowakabili watoto waliotoka mgongo nje pamoja na vichwa vikubwa, unaelezwa kusababishwa na ukosefu wa Folic Acid mwilini, hali inayochangiwa na mama mjamzito kupenda kula chipsi kuku.Daktari wa Hospitali ya Taifa ya Muhimbili, wodi ya watoto ya Moi, Agricore Joseph alisema wanawake wengi hufikia hatua ya kujifungua watoto wenye matatizo hayo kutokana na kupenda vyakula hivyo, kitu ambacho kinaweza kuepukika.

Mtoto akiwa na uvimbe mgongoni. “Nakujua wewe ni MC maarufu, huko unakopita jaribu kuwaelimisha wanawake juu ya tatizo hilo, na wewe Nuru kwenye kile kipindi chako waelimishe wanawake juu ya hili, naamimi tunaweza kupunguza idadi ya wanaojifungua watoto wenye tatizo hili,” alisema daktari huyo.Alisema, ni wakati sasa wanawake hasa wajawazito kuelimishwa juu ya kutopendelea chipsi kuku badala yake kutumia vyakula ambavyo vinaongeza Folic Acid na kunywa vidonge vinavyotolewa kliniki.

BIBI YAKE OBAMA AJISAHAU KULA AKIMSHANGAA MJUKUU WAKE RAIS OBAMA,

$
0
0

RAIS OBAMA AKILA CHAKULA NA FAMILIA YAKE.

MJUE RAIS ANAYEONGOZA KUTOKUWA NA ELIMU YA SHULE KABISA KATIKA AFRICA LIVE!1

$
0
0


1. Jacob Zuma- Republic of South Africa Zuma received no formal schooling. The debate surrounding South African president Jacob Zuma’s lack of formal education has been a hot discussion topic for years.Prince Mashele, CEO of the...
Africa Cradle

NYOKA AKUTWA AKITOA PESA KWENYE ATM ZA BENKI YA BARCLAYS!

$
0
0
On Saturday a strange accident happened in Harare, Zimbabwe. According to the report a snake slithered to an ATM machine at Barclays Bank Angwa Street and then entered a car.
Passers-by surrounded the car to get a closer view of the snake and its owner. Others were busy taking photos from the onset and managed to capture pictures of the snake and the car that it later entered.Social media was awash with pictures of the incident. A large crowd of onlookers had also gathered to see what was going on.
 





When the crowd mobbed the car and asked the driver to explain the bizarre occurrence, he professed ignorance and unperturbedly asked them to release him so he could go home. He said: “I don’t know what you are talking about, let me go home”. 

  
 BONYEZA HAPA KUONA VIDEO YA  TUKIO HILO

HAYA NDIO MAMBO YA MOMBASA KWENYE SHUGHULI ZAO

$
0
0
Mombasa ni kati ya miji siyoisha shughuli kila siku, kama tu huku kwetu maeneo ya pwani. Tatizo ni moja kwenye shughuli watu
hupandisha sana mizuka hadi kuvua nguo hata kubaki watupu na kuanza kukatika.

BONGO MOVIE HAKUKALIKI SASA BAADA YA WEMA KUBWAGWA UNAJUA KILICHOMKUTA UWOYA?

RAIS GLOBAL PEACE FOUNDATION TANZANIA DR. SALEM ABDULLA ALIPOAGANA NA MARAIS NA MAWAZIRI WA NCHI 20 ZA DUNIA LEO ASUBUHI ZANZIBAR LIVE!

$
0
0
 Mkutano huu ulihudhuriwa  na nchi 20.na mabalozi.marais.wabunge. viongozi wa dini mbali mbali. Dr. Salem Abdulla rais wa Global Peace Foundation Tanzania leo asubuhi baada ya kukifunga rasmi kikao cha semina kilichofanyika Zanzibar kilichowakutanisha Marais wa sasa na wa zamani wa Nchi kadhaa za KiAfrika na pia Viongozi wa Dini.
 
      semina ilihudhuriwa kwa muda mchache na mgombea Urais mteule wa CCM Dr. Magufuli ambaye alipitia hapo kumuona rafiki yake wa karibu sana Waziri Mkuu wa zamani wa Kenya Bw. Raila Odinga

WASSIRA AMTWANGA NA KUMJERUHI MWENYEKITI WA CCM MKOA WA MARA

HOME SWEEET HOME RAIS WA DUNIA ALIPOKUTANA NA NDUGU ZAKE WA DAMU KENYA LIVE!!

$
0
0

'Welcome home, Mr President': Obama's all smiles as he catches up with long-lost family on official visit to Kenya 

  • President met Auma Obama as he landed in Nairobi late Friday night
  • Was also greeted by Kenyan president Uhuru Kenyatta and other officials
  • Was whisked into capital city in a motorcade ahead on five-day Africa visit 
  • Went to family meal in his Nairobi hotel and sat next to step-grandmother 
  • Obama will also visit Ethiopia after three days in Kenya 
Not long after touching down in Nairobi, Obama was taken to a hotel where he met fellow Obamas including his half-sister and step-grandmother.
The President was seen smiling at a table between Mama Sarah Obama, whom he calls 'granny', and Auma Obama, who was born to his father's first wife.
Beaming: A happy Barack Obama joined a family dinner with his step-grandmother Mama Sarah, to his left, and half-sister Auma, to his right, at a family meal in Nairobi, Kenya
Beaming: A happy Barack Obama joined a family dinner with his step-grandmother Mama Sarah, to his left, and half-sister Auma, to his right, at a family meal in Nairobi, Kenya
State occasion: The family gathering came as Obama made his first visit to Kenya as president
State occasion: The family gathering came as Obama made his first visit to Kenya as president
Big meeting: Obama went to the meal in Nairobi at the hotel where he was staying soon after landing in the capital
Big meeting: Obama went to the meal in Nairobi at the hotel where he was staying soon after landing in the capital
Some three-dozen people were at the meal sitting round the President at the Villa Rosa Kempinski hotel, where he is staying on his brief visit to the country.

The luxury property can accommodate some 500 diners and has a host of restaurants as well as a plush presidential suite on its tenth floor. He headed straight to the family occasion after disembarking from Air Force One late Friday night, where he was met by Auma as well as a group of high-ranking Kenyan officials.

Included among them were president Uhuru Kenyatta, who joked with Obama as he sat at a desk rolled up in front of the presidential plane and signed a visitors' book for the nation.

Crowds of excited citizens crowded as close as possible to his heavily-guarded route and welcome him to their country.
Family reunion:  Obama is pictured above at Bairobi's airport hugging Auma, who met him along with the Kenyan president, Uhuru Kenyatta, right in a yellow tie
Family reunion:  Obama is pictured above at Nairobi's airport hugging Auma, who met him along with the Kenyan president, Uhuru Kenyatta, right in a yellow tie
Together: Obama and Auma met when the president was a young man living in Chicago
Together: Obama and Auma met when the president was a young man living in Chicago
Shooting the breeze: Obama shares a joke with Kenyatta, as he signs a visitors' book on a desk set up in front of his plane
Shooting the breeze: Obama shares a joke with Kenyatta, as he signs a visitors' book on a desk set up in front of his plane
Gift: Obama was given a bouquet of flower by Joan Wamaitha, and eight-year-old Kenyan girl, on his arrival 
Gift: Obama was given a bouquet of flower by Joan Wamaitha, and eight-year-old Kenyan girl, on his arrival 
Hours before Obama's arrival, police blocked major roads and emptied streets of traffic in the usually congested capital as part of a huge security operation. 


SUPER STAR DIAMOND PLATINUMZ ANYAKUA TUZO NYINGINE HUKO SOUTH AFRICA!

$
0
0
Diamond Platnumz akiwa na Meneja wake Sallam ndani ya SouthAfrica
Msani wa Tanzania katika miondoko ya Bongo fleva Diamond Platnumz (@diamondplatnumz) ameshinda tuzo ya ‘African Achievers Awards’ katika tuzo zilizotolewa na kufanyika nchini Afrika kusini, Tuzo aliyoshinda Diamond ni yaArtist of the Year ‘Msanii Bora Wa Mwaka’.
Diamond Platnumz Akiwa ameshika Tuzo yake aliyoshinda SouthAfrika kama Msanii bora wa Mwaka

MY SUPER FRIEND SUPER MODEL MELINA OBARE LIVE FROM MBELEZ DC WASHINGTON ONA LE MBEBEZ!!

PICHA 8 ZAIDI ZA RAIS WA DUNIA ALIPORUDI HOME KWA MARA YA KWANZA TOKA AWE RAIS WA USA MAPAKA RAHA MWANANGU!!

$
0
0
Rais wa Dunia Obama akipokewa na Rais wa Kenya Uhuru Kenyatta baada ya kutua home!!







LE BIG SHOW LIVE WITH MY PEOPLE WE ARE ALL HUMBLED!!!

$
0
0
From Left:- Movie Star Richie Mtambalike + Super Star Singer QChief + Le Mutuz Nationa + Movie Star JB + Super Star Comedian Massanje Mkandamizaji live at Leaders Club!!



DADA HUYU KUTOKA CHIMBO HOTEL ANAWANYIMA VIDUME USINGIZI WENGI WAMFUATA KWA PESA ILI WAMPATE LAKINI KUMBE MTOTO ANAPENDA

$
0
0



This Is The Super Sexy Girl With Curves To K!ll From Chimbo 12 Hostels That Is Giving Men

Sleepless Nights....They Have Emptied Their Pockets Trying To Impress Her!!   

Viewing all 32622 articles
Browse latest View live


<script src="https://jsc.adskeeper.com/r/s/rssing.com.1596347.js" async> </script>