Quantcast
Channel: Blogu ya Wananchi
Viewing all 32622 articles
Browse latest View live

LE MUTUZ NATION MY ONE DAY STAY LIVE AT ZANZIBAR THE DOUBLE TREE HILTON HOTEL THE PLACE TO BE!!


LE BIG SHOW BUSINESS SUPER LUNCH AT THE DOUBLE TREE HILTON HOTEL WITH SUPER LAWYER ROSE MUKAREEZZZ U KNOW LIVE!!

TEAM WEMA WAMCHARUKIA DIAMOND BAADA YA KUTOA MANENO MACHAFU KWA WEMA BAADA YA WEMA KUSHINDWA UBUNGE

$
0
0
This are 10 statement from Wema Sepetu about her x-boyfriend Diamond Platnumz!! You cant believe how she appreciate and respect Diamond Talent's!! MUST READ.


Few month ago actress and former miss Tanzania wema sepetu speak out about his x-boyfriend at EFM radio program known as Ubaoni and this is the ten statement she made about diamond platnumz.

DIAMOND PLATNUMZ ASHINDA TUZO NYINGINE AFRIKA KUSINI ‘AFRICAN ACHIEVERS AWARDS’.

$
0
0

Msani wa bongo fleva Diamond Platnumz ameshinda tuzo ya ‘African Achievers Awards’ katika tuzo zilisofanyika Afrika kusini, Tuzo aliyoshinda Diamond ni ya Artist of the Year ‘Msanii Bora Wa Mwaka’.

DEREVA WA BAJAJI ALETA VURUMAI MTAANI.

LE MUTUZ NATION MY ONE DAY STAY IN ZANZIBAR JANA LIVE AT THE MARUHUBI BEACH WITH SIMBA SPORTS NEW COACH LIVE!!

$
0
0
Le Big Show on the Way to Zanzibar on Zan Air live!!

Le Big Show live at the Maruhubi Beach with Super Star Actress Shamsa Ford live!!




Le Big Show with Mr. Kerr Simba Sports Club new Coach live at Maruhubi BEach


Le Big Show hanging out with Simba Sports Assistant Coach Mr. Dulley live at Maruhubi Beach Zanzibar!!


Le Big Show chilling with from left Super Star Actress Shamsa Ford + Super Star Actress Davina + Le Mutuz Nation + Kajala's Manager Lamata + Super Star Actress Eshasbuheti live jana at Zanzibar!!





JINA LA RAIS LASAMBAA MTAAANI.

$
0
0
Nchini Kenya watoto sita waliozaliwa siku ya kuamkia jumamosi apewa jina la rais wa Marekani Obama.Rais Obama yupo toka siku ya ijumaa nchini humo kwa ziara ya siku nne.

LE SUPER SUNDAY NA MTANGAZAJI MAARUFU.

$
0
0
PICHA MATATA YA MTANGAZAJI MAARUFU WA KIPINDI CHA MAPENZI ASIYE HATA NA DOA USONI.

TAFAKARI YA KIPANYA LEO.

MWANASHERIA MAARUFU MH. UMMY MWALIMU ASHINDA KWA KISHINDO UBUNGE VITI MAALUM TANGA LE MAFURIKOZZ LIVE!!!!

$
0
0

NIMEHEMEWA! Wanawake wa UWT/CCM Mkoa wa Tanga wameonyesha imani kubwa sana sana kwangu kwa kunipa kura 786 kati ya kura 793 ili kuwawakilisha Bungeni 2015 - 2020.


Ninapenda kutumia ukurasa huu leo KUWASHUKURU kwa dhati wana UWT wa Wilaya zote za Mkoa wa Tanga kuanzia Kilindi, Handeni, Lushoto, Korogwe Vijijini, Korogwe Mji, Muheza, Pangani, Mkinga na Tanga Mjini. NINA DENI KUBWA SANA KWAO. Ninawaahidi Utumishi uliotukuka ktk kusukuma mbele maendeleo ya wanawake na watoto wa Mkoa wa Tanga. Narudia kusema tena "NIMEHEMEWA". Alhamdulillah. Sasa ni Mbele kwa Mbele ktk kutafuta ushindi wa CCM kwa nafasi ya Rais, Wabunge na Madiwani 25 Oct 2015.
-----
Matokeo UWT mkoa wa Tanga

Kura zilizopigwa 797. Kura zilizoharibika 4. Kura Halali 793.
1. Ummy Mwalimu 786 (99.1% ya kura zote)
2. Sharifa Abebe 431
3. Aisha Kigoda 118
4. Saumu Bendera 91
5. Sophia Mhilu 84
6. Laicky Gugu 52
7. Josephine Mgaza 8
8. Asia Kalage 7
9. Farida Mashaka 7
10. Angella Mganga 3


Hivyo waliopitishwa nafasi ya Ubunge Viti Maalum Wanawake/CCM Mkoa wa Tanga ni Ummy Mwalimu na Sharifa Abebe.

HII NDIO SABABU YA VIJANA WENGI KUPOTEZA MUDA NA BANDO HUKO INSTAGRAM>

$
0
0
Instagram Crush: This is why I spend my time on Instagram....








USIOMBE YAKUKUTE YALIYOMTOKEA MREMBO HUYU

$
0
0
MAMBO mengine ni ya kuyasikia yakiwatokea wenzako na usiombe yakakukuta kama ilivyomtokea msichana huyu ambaye hakufahamika jina lake mara moja baada ya kuchukua kipigo ‘hevi’ ambacho nusura apoteze maisha yake, maeneo ya Sinza Afrikasana, juzi Jumatatu.

Dada huyo akilia baada ya kupokea kichapo kikali.

Mashuhuda wa tukio hilo wanasema, binti huyo akiwa na mwanaume mmoja, walionekana wakitoka katika baa iitwayo Kona, wakiongozana hadi kwenye baa nyingine iliyo maeneo ya Afrikasana ambako waliendelea na kinywaji.
“Yule msichana ni mmoja wa wanaojiuza pale Kona, nadhani walikuwa na makubaliano ambayo wamefikia, maana walikuwa wakinywa kwa raha zao, ghafla tukasikia wanaanza kuzozana, jamaa alikuwa anataka waondoke, bibie akawa analeta longolongo,” alisema dada mmoja aliyekuwa eneo la tukio.
Wasamalia wema wakimsaidia.
Inadaiwa kuwa dada huyo alianza kupiga yowe akitaka apewe kiasi cha shilingi 30,000, ndipo mwanaume huyo ambaye alitoweka haraka, alipoamua kumpa kipigo kikali kiasi cha kumpasua kichwani na kumsababishia maumivu makali.
Akiwa amelala.
Baada ya kupokea kipigo hicho, baadhi ya wahuni walifika eneo hilo na kuendelea kumfanyia vitendo vya kidhalilishaji hadi akina mama wa eneo hilo walipoamua kumhifadhi kwa kumfunika kanga, lakini katika hali ya kushangaza, msichana huyo alipitiwa na usingizi mzito.Kuona hivyo, majirani hao waliamua kumpeleka polisi ambako hata hivyo alifukuzwa kwa kile kilichodaiwa kuwa ni mlevi.

UKAWA WAITA WAHARIRI WA VYOMBO VYA HABARI LEO SAKUMI JIONI

$
0
0

JUMUIKO la vyama vinavyounda muungano wa kutetea katiba ya Wananchi (UKAWA), linatarajiwa kumtangaza mgombea wake urais jioni hii, jijini Dar es Salaam.

Taarifa kutoka ndani ya umoja huo zinasema, mgombea urais wa UKAWA aweza kupatikana leo, baada ya mashauriano ya kina yaliyofanyika baina ya viongozi wakuu wa vyama vinavyounda umoja huo.

“Jioni hii ya leo, tutakuwa na mkutano na waandishi wa habari kwa lengo la kumtangaza mgombea wetu wa urais. Tutatangaza moja kwa moja mgombea au tutakitangaza chama ambacho kitatoa mgombea,” ameeleza mmoja wa viongozi wakuu wa UKAWA kwa sharti la kutotajwa gazetini.

Amesema, “ikiwa tutakitangaza chama, basi kitakachofuata, ni kukiruhusu kuendelea na mchakato wake wa ndani. Lakini katika hayo mawili, moja lazima litafanyika – tutangaza mgombea au chama kitakachotoa mgombea.”

Mkutano wa viongozi wakuu wa UKAWA unaotarajiwa kutangaza mgombea wake urais, umepangwa kufanyika katika hoteli ya Bahari Beach.
Vyama vinavyounda muungano wa UKAWA, ni NCCR- Mageuzi, Chama cha Wananchi (CUF), Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) na National Democrat Party (NLD).

Kwa mujibu wa mtoa taarifa wa gazeti hili, chama ambacho kitatoa mgombea urais wa Muungano, kimetajwa kuwa Chadema. Mgombea urais wa Zanzibar, atatoka CUF.

Anasema, makubaliano kuwa Chadema ndicho kitoe mgombea urais wa Muungano tayari yameridhiwa na Baraza Kuu la Uongozi la CUF, lililokutana mjini Zanzibar jana Jumamosi.

Wachambuzi wa mambo ya kisiasa wanasema, hatua ya CUF mmoja wa washirika wakubwa katika umoja huo kuridhia Chadema kutoa mgombea urais, limekuwa pigo kubwa kwa wapinzani wa muungano huo.

“Haya mawili ya rais wa Muungano na rais wa Zanzibar, tayari tumekubaliana. Chadema kitatoa mgombea urais wa Muungano na CUF kitatoa mgombea mwenza. Mbali na mgombea mwenza, CUF kitatoa pia mgombea urais wa Zanzibar,” anaeleza kiongozi huyo.

Hata hivyo, taarifa kutoka ndani ya Chadema zinasema, chama hicho kinaweza kuzuia kumtangaza mgombea wake wa urais katika mkutano wa leo na waandishi wa habari, ili kukamilisha mazungumzo yake ya ndani.

Kinachoitwa na chama hicho, “mazungumzo ya ndani,” kimetajwa na afisa mmoja wa Chadema kuwa ni suala la kuchelewa kupatikana jina la mgombea mwenza kutoka CUF.

Aidha, taarifa zinasema, kushindwa kwa chama hicho kumtangaza mgombea wake urais wa Muungano, kunatoka pia na kutokamilika kwa “mashauriano” kati yake na mmoja wa watu muhimu nje ya chama hicho.”

Lakini kwa zaidi ya wiki mbili sasa, vyombo vya habari vimenukuu vyanzo mbalimbali vya taarifa vikieleza, anayesubiriwa na Chadema kutoka nje ya chama, ni mbunge wa Mondoli (CCM), Edward Lowassa.

Taarifa kuwa Lowassa, mmoja wa wanasiasa machachari nchini, anataka kujiunga na Chadema, zimepamba moto katika wiki za hivi karibuni baada ya jina lake kuenguliwa katika hatua za awali katika kinyang’anyiro cha urais kupitia CCM.

Tayari madiwano 20 na viongozi wengine mbalimbali wa CCM wamekihama chama hicho na kujiunga na Chadema, jambo ambalo limeashiria kukamilika kwa safari ya kiongozi huyo ndani ya Chadema.

MREMBO AACHIA PICHA ZAKE MATATA

$
0
0


 

Sabby Angel  Decides to Flaunt her Assets for Tanzanian  MEN













JK APATA TUZO YA UTAWALA BORA!

$
0
0
RAIS Jakaya Kikwete ametunukiwa tuzo na Taasisi ya African Achievers Awards, yenye makao makuu Afrika Kusini, kwa kutambua mchango wake katika kuimarisha, kuendeleza na kudumisha Utawala Bora, kwa miaka 10 ya uongozi wake.

Taarifa ya Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais, ilisema Kikwete anaungana na watu wengine wachache waliowahi kupokea tuzo hiyo tangu ilipoanzishwa na kutolewa kwa mara ya kwanza kwa Askofu Mkuu wa Kanisa Anglikana la Afrika Kusini, Desmond Tutu, mwaka 2011.
Askofu Tutu alipewa tuzo kufuatia mapambano yake kutetea haki za binadamu, usawa na amani.

Kwa mujibu wa taarifa hiyo, Rais Kikwete ameteuliwa kutoka miongoni mwa watu zaidi ya 1,202, ambao majina yao yaliwasilishwa kwenye Jopo la Kimataifa linalojitegemea,lenye wajumbe kutoka Uingereza na Afrika Kusini, waliokaa na kufanya uteuzi.
Ilisema, kutokana na tunuku hiyo, Rais Kikwete alialikwa Afrika Kusini kupokea tuzo hiyo, kwenye sherehe iliyofanyika jana katika Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Sandton, mjini Johannesburg.
Hata hivyo, kutokana na kukabiliwa na shughuli nyingi nyumbani, Rais Kikwete amewakilishwa na Waziri wa Katiba na Sheria, Asha-Rose Migiro, kwenye sherehe ya kupokea tuzo hiyo, ambako pia atatoa mada kuhusu “Umoja wa Afrika: Fursa na Changamoto (Africa’s Unity: Prospects and Challenges) “ kwa niaba ya Rais Kikwete.
Tuzo za African Archievers Awards zinalenga kuwatambua watu binafsi na taasisi ambazo zimejitambulisha kwa michango yao kwa ustawi na maendeleo ya Bara la Afrika.
Mtendaji wa African Achievers Awards, Rex Indaminabo katika barua ya kumjulisha Rais Kikwete kuhusu uteuzi huo alisema, “ Uongozi wa African Achievers Awards unayo furaha kukujulisha juu ya uteuzi wako wa kupokea tuzo ya 2015 African Achievers Awards katika kundi la Utawala Bora Barani Afrika".
"...Ni kwa furaha na heshima kubwa kuwa wajumbe wa Bodi ya Ushauri na Taasisi ya Uongozi na Menejimenti wanakuandikia kukupongeza kwa kuteuliwa kwenye orodha ya mwisho na hatimaye kuwa mshindi wa Tuzo ya African Achievers Awards katika kundi la Utawala Bora katika Afrika.”

JACOB STEPHEN AANZA MAZOEZI AKUTANA NA AKINA WARIDI, MONALISA NA NATASHA!

$
0
0
NI mfululizo wa simulizi ya maisha ya staa nguli katika fani ya uigizaji, Jacob Stephen Mbura ‘JB’. Hakika ni simulizi tamu iliyojaa mafunzo, hamasa na burudani kwa baadhi ya maeneo. Wiki iliyopita, tuliishia pale msanii huyo alikubali kujiunga na fani ya uigizaji baada ya kupata ushawishi mkubwa kutoka kwa msanii Single Mtambalike ‘Richie’ pamoja na shinikizo la mama yake mzazi.
Hata hivyo, alipofika eneo walilokuwa wakifanyia mazoezi, akasikia sauti zikitokea ndani na alipochungulia, alichokiona hakutaka tena kuendelea kukitazama. Kufikia hapo akawa ameamua kufuta kabisa wazo la kufanya sanaa.
Je, JB aliona nini siku hiyo? Ungana nami hapa chini uzidi kujifunza mengi kuhusu vita ya maisha.

“Yalikuwa ni mazoezi makali ambayo licha ya kupitia mafunzo ya kijeshi, sikuwahi kuyaona mahali popote, yalinitia hofu mno,” anasema wakati akikaa vizuri kwenye kiti.

“Nikaona kama ni upotevu wa muda tu, nikalinganisha kazi yangu ya biashara ambayo ilikuwa ikiniingizia kipato na mazoezi hayo nikaona ni heri niendelee na biashara,” anasema.
“Kichwani nikaamua kwa dhati kabisa kufuta mambo hayo, nikajiandaa hoja nzito za kukabiliana na ushawishi wa Richie na mama yangu mzazi.

“Lakini waliendelea kunishinikiza kujiunga na mazoezi yao, pamoja na wakati mwingine kumtolea lugha chafu na za maudhi, lakini Richie hakukata tamaa wala kuvunjika moyo juu ya kunishawishi nifanye sanaa, sijui alikuwa akinifikiria nini,” anasema JB.

“Na hapa, ngoja niseme jambo ambalo moyo wangu unanishtaki kwao, jambo lenyewe ni kuhusu Richie,” anasema JB huku akitazama juu akiwa amekunja ndita, anavuta pumzi ndefu na kuzishusha taratibu.

“Katika mafanikio yangu ya maisha ya uigizaji, tena hata maisha kwa ujumla, hakika siwezi kumsahau Richie, huyu ni babu katika sanaa ya filamu, wewe mwangalie hivyohivyo tu,” anasema JB lakini awamu hii kwa sauti ya juu kabisa.
“Unajua hata jina la Ray, Vincent Kigosi alipewa na nani? Ananiuliza JB akiwa amenikazia macho na kabla sijajibu chochote, haraka sana akaniwahi na kunipa jibu.

“Ni Richie, kwa taarifa yako ni Richie. Sikiliza, kwangu mimi Richie ni zaidi ya msanii na rafiki, huyu ni mwalimu wangu, mhamasishaji wangu na hata ushirikiano wetu katika mambo mbalimbali ya kimaisha, hauishii kwenye filamu tu, hata mambo mengine,” anasema mfululizo JB.

“Richie ameendelea kuwa mtu muhimu sana maishani mwangu, hata familia yangu inalitambua hilo, namshukuru sana Mungu wa mbinguni kwa kunikutanisha na Richie, ni mtu sahihi katika safari yangu ya mafanikio, Mungu ambariki babu Richie,” anasema huku akionesha tabasamu hafifu kwa mbali.

“Basi bwana, Richie akaendelea na ushawishi wake hatimaye nikaamua tena kuanza kuigiza, nikaanza mazoezi, wakati huo kundi lao lilikuwa likijulikana kwa jina la Nyota Assemble,” anasema.

“Miongoni mwa wasanii niliowakuta ni pamoja na Richie mwenyewe, Waridi, baadaye wakaja akina Monalisa, Natasha, akina Mjomba Fujo na Seki, wengine siwakumbuki maana imekuwa ni muda kidogo,” anasema JB.
“Shughuli ikaendelea, nikaambiwa kufanya mazoezi kwa muda mrefu huku nikipewa mafunzo maalum, pamoja na mbinu mbalimbali za kuigiza, hakika nikaanza kuzoea ugumu wa mazoezi na kujikuta nikiwa mzoefu kabisa,” anasema kisha kuachia kicheko.

“Lakini pia, hapa nataka niseme jambo lingine muhimu sana kuhusu sanaa yetu, sijui katika makundi mengine lakini Kundi la Nyota Assemble, hakika lilikuwa kundi la kipekee sana,” anasema.

“Si tu kwamba tulijifunza kuigiza peke yake, lakini tulifundishwa nidhamu, heshima na mambo mengi sana juu ya maisha, kitu ambacho nakiona kwa wasanii wachanga hakipo,” anasema JB huku akionesha sura ‘ngumu’ kidogo.
Je, nini kitaendelea? Usikose kufuatillia wiki ijayo kwa uhondo zaidi

DAR LIVE ILIVYOTIKISWA NA RAP FESTIVAL JANA

$
0
0
Roma akifanya yake.
Darasa akilikabili jukwaa.


Stamina akichana.Izzo Bizness akifanya yake.
Young Dee akipozi mbele ya mashabiki.
Mwanadada anayekuja kwa kasi kwenye Hip Hop aitwaye Chemical,  akichana.
Niki wa Pili akijiandaa kwa makamuzi.Barakah Da Prince akiwalainisha mashabiki.Dj D. Ommy  (wa kwanza kulia) akirekebisha mitambo kabla ya shoo kuanza.
Umati wa mashabiki wa Hip Hop ukifuatilia kwa makini burudani hizo.
KAMA kawaida Ukumbi wa Taifa wa Burudani wa Dar Live ulioko Mbagala-Zakhem jijini Dar es Salaam, jana ulitikiswa na tamasha la Muziki wa Hip Hop lililopewa jina la Rap Festival ambalo liliwakutanisha wasanii mbalimbali wa Hip Hop ana kwa ana na mashabiki wao.
Tamasha hilo lililoanza mishale ya saa tano usiku kwa wasanii chipukizi kupanda jukwaani na kuonesha uwezo wao wa kuchana, lilifunguliwa rasmi na mshereheshaji ambaye pia ni mkali wa Hip Hop, Adam Mchomvu,  huku muziki ukisimamiwa na Dj D.Ommy.
Mashabiki wa Hip Hop walishuhudia mastaa kibao wakilishambulia jukwaa kwa staili tofauti-tofauti na kufanya burudani isiwachoshe zaidi ya kuwaburudisha.
Baadhi ya wasanii waliopanda jukwaani hapo ni Stamina, Niki wa Pili, Roma, Stamina, Young Killer, God Zilla, Adam Mchomvu, Nikki Mbishi, Climax, Darasa, Izzo Bizness, Young Dee, Chemical na Chiku Kheto.
(Picha/ Chande Abdallah na Deogratius Mongela)

UBUNGE VITI MAALUM: WAKATI WEMA SEPETU ANALIA, MWANAMUZIKI KEISHA ANACHEKELEA

$
0
0
Ksher 1
2015 tumeshuhudia mastaa mbalimbali wa kike na wa kiume Tanzania wakitangaza nia ya kuingia bungeni akiwemo mwimbaji wa Taarab Mzee Yusuf, Profesa Jay, Steve Nyerere na kwa Wanawake waliojitokeza kuziwania nafasi za Ubunge wa viti maalum ni pamoja na waigizaji Wema Sepetu na Wastara, na msanii wa bongofleva Ksher.

Wema Sepetu na Wastara hawakupita kutokana na kukosa kura za kutosha lakini Khadija Shaaban (Ksher) amepita tena ambapo alithibitisha hayo na wakati mwingi kwenye maneno yake ya kujinadi ni ‘mara nyingi watu wanakosa uthubutu kutokana na kutojiamini kuwa vile walivyo wanaweza kufanya mambo makubwa ya ajabu bila kujali kiwango cha elimu, pesa au mtandao alionao’
Ksher 2
Kwa upande wa Wastara, kwenye kura za maoni zilizopigwa akiwania Ubunge wa viti maalum kupitia Walemavu, zilipigwa kura 759, zikaharibika 40 huku Magreth Mkanga akipata kura 424, Wastara akishika nafasi ya pili kwa kuchukua kura 254 na Chausiku Lukinga 43.

Wastara

LE MAJANGAZ JIONEE ALICHOPOST MREMBO HUYU LIVE

Picha,Baada ya kutimiza miaka 46, Jennifer Lopez Kavalia hili vazi kuonyesha hajazeeka.

$
0
0
Jennifer-Lopez
Ilikuonyesha watu kuwa hajazeeka msanii wa pop Jennifer Lopez  alivalia vazi hili kwenye sherehe fupi ya siku yake ya kuzaliwa wekend hii. Jennifer amefikisha miaka 46.

JLo alikuwa na mpenzi wake Casper Smart mwenye miaka 28 na rapa French Montana .
j lo
j lo 2 j lo 3
Viewing all 32622 articles
Browse latest View live


<script src="https://jsc.adskeeper.com/r/s/rssing.com.1596347.js" async> </script>