Quantcast
Channel: Blogu ya Wananchi
Viewing all 32622 articles
Browse latest View live

MBONGO MBEBEZZ AWASHA MOTO WA BUSINESS MBELEZZZ USA ANAITWA "MAMA ALASKA" MUONE HAPA LIVE!!

$
0
0

@mrproblemsolved with @repostapp.
・・・
Kibiashara anajulikana kama Mama Alaska, ila watu wake wakaribu wanamjua kama Jennifer Bash.
Mie namuita Mama Future Billionaire!


Jennifer ni mjasiriamali wa kipekee. Anachapa kazi kama mwendawazimu (umkute amekaa anafungasha order ya TANI NZIMA ya mchele kwenye mifuko ndo utaelewa kwanini nasema hivyo), jambo ambalo linaniacha nakohoa kwenye vumbi ukizingatia kwamba YEYE NI MKE WA MTU NA MAMA WA WATOTO WATATU PIA!

Bidhaa zake za MCHELE, MAYAI NA MAFUTA YA KUPIKIA ZINAPATIKANA KWA JINA LA ALASKA TANZANIA kwenye supermarket 7 tofauti zenye branch 24 kwa ujumla.
Nina wateja karibu 190, wengi wanawake, ila sijawahi kuona mtu mwenye njaa ya mafanikio kama Jennifer. Mpole, mcheshi, msikivu na HATAKI KUBAKI MDOGO hata kama alianza mdogo.
Wakati namfungia Minishop System kama mwaka na nusu uliopita, alikua anauza mayai tu.

Minishop System ikamsaidia kuweka mahesabu yake kwenye msingi imara, akawa anaelewa anachokifanya na hatimaye akaja kuzindua mchele wa Alaska Tanzania ambao unauzika kama maji kutokana na ubora wake na usafi wa packaging yake.
Badala ya kuishia hapo, wiki kadhaa zilizopita tulikaa kuongea akanionyesha bidhaa yake mpya ya mafuta ya kupikia!
@mama_alaska hachoki kuleta jipya na kwavile biashara yake inaendeshwa kwa kutumia Minishop System, Jennifer habatishi kwenye mahesabu, jambo ambalo ndani ya miaka mitano ijayo litamfanya awe Bhakresa wetu wa kike. 100%

Kujipatia Minishop System nawewe CHUKUA SIMU YAKO hapo sasa hivi umpigie Joseph 0756-89-59-89 au Apendaeli 0782-519-063 au Upendo 0788-735-669.

Jennifer aka @mama_alaska @mama_alaska @mama_alaska @mama_alaska @mama_alaska @mama_alaska ninavyosema WANAWAKE WANAWEZA wewe ni dhibitisho tosha. Mungu akuzidishie uje usambaze bidhaa za Alaska Tanzania kwenye kila nchi DUNIA NZIMA 💪💪

KIGOGO WA CCM AFUNGUKA KWA MARA YA KWANZA KUHUSU LOWASA NA CCM NA KUELEKEA KWAKE CHADEMA LIVE!!

$
0
0

Kauli ya Juma Volter Mwapachu Kuhusu Lowassa
Nimekuwa kimya kwa muda mrefu katika mabadilishano ya fikra kwenye mtandao huu ambao kwa hakika, kwa maoni yangu, haubidi kuwa ni wa fikra pevu zisizo shawishika na misimamo ya 'kimalaya ya siasa'.
 Kama tutaserereka katika msingi huu, basi ni bora Chambi ukafunga virago na kusitish huu mtandao. Nimesoma mabadilishano na mabishano ya fikra kuhusu hali ya siasa nchini mwetu na hususa ni baada ya Mhe Lowassa kuamua kujiunga na Chadema na kuwa mwakilishi wa UKAWA katika kinyang'anyiro cha nafasi ya Urais wa Jamhuri ya Muungano. Sijui nyie wenzangu  mmesimamia wapi katika suala hili.
Naomba niseme mwanzoni kabisa kwamba nchi yetu hii leo imefikia mahali ambapo wasomi, wanazuoni kama sisi katika mtandao huu, Hatuna budi kujitokeza na kuhesabika tunamuunga nani mkono katika uchaguzi ujao wa Rais wa Tanzania. Tuwe wakweli na siyo kuendelea kuegemea katika kificho cha 'uhuru' wa wanazuoni katika kutoa maomi na fikra kama vile sisi si wapiga kura au wananchi wanaothamini umuhimu kuhusu uongozi wa nchi yetu. Wakati huo umepitwa na hali halisi ya itikadi na maana muhimu ya uongozi wa Taifa.
Sasa, Mimi binafsi, namuuunga mkono Edward Ngoyai Lowassa. Yako mengi ambayo kazuliwa huyu ndugu yetu; tunaambiwa tangu 1995 wakati Mwalimu Julius Nyerere alipotamka kwamba 'huyu kijana ninalo faili lake, ana utajiri usiyoelezeka. Ana nyumba kadhaa.' Lakini huyo huyo Baba wa Taifa alimpenda sana Edward na kumpa madaraka ndani ya CCM na baraza la mawaziri. Kama Edward alikuwa 'corrupt' swali ni kwanini Baba wa Taifa hakumchukulia hatua za kisiasa na kisheria? Kwanini aseme hayo aliyoyasema mwaka 1995 wakati Edward Lowassa alikuwa akiongoza kupendwa dani ya CCM, ngazi zote na akitarajiwa ndiye angependekezwa kuwa mgombea wa Urais? Jamani, wanazuoni, lazima mtafakari historia na hali halisi ilivyokuwa. Mhe Jakaya Kikwete hakuwa 'the favourite' candidate in 1995. Na Mwalimu alimtaka Ben Mkapa wakati ule awe Rais. Ilibidi Lowassa atoswe kinamna!
Mimi namfahamu Edward, Ninyi mnaujua huo utajiri wake au basi akitoa michango hapa na pale ni pesa zake? Kati yenu mna utajiri zaidi ya Edward. Edward alivumilia na kumsaidia mwenzake (nasita sasa hivi kutumia neno 'rafiki') Jakaya ashinde uteuzi wa mgombea wa CCM hapo 2005. Aliamua hivyo baada ya makubaliano ya 1995. Wapo wengi wa Tanzania waliyojitolea muhanda, wa hali na mali kuungana na Edward kumwezesha Jakaya Kikwete kuwa Rais 2005. Kati yao, ndiyo wamekuwa karibu na Edward katika kinyang'anyiro cha majuzi Dodoma. Imani yao ilikuwa kwamba pamoja na mkanganyiko wa Februari 2008 wa Richmond ambao hauna mashiko yoyote ya ufisadi kwa maana ya rushwa, Rais Kikwete angemfungulia mlango mwenzake Edward kuwa mgombea wa CCM. Badala yake Edward bado akajengewa mzengwe wa utajiri kama Baba wa Taifa alivyofanya 1995. Hivi leo tukichambua nani kati yetu ni tajiri zaidi ya Lowassa tutakuwa na viongozi wanao kidhi mategemeo yetu?
Kuhusu hili swala la Richmond: Hivi baada ya taarifa ya Tume ya Bunge ya Dr Mwakyembe, Serikali ilitoa majibu. Mbona kwenye tuhuma za Bunge kuhusu Tegeta Escrow imekuwapo taarifa toka kwa Chief Secretary kuhusu suala hilo? Nani aliyejaribu kutoa maelezo ambayo yangemfungisha Lowassa au kumkomboa kwa kitendo chake cha kujiuzuru kisiasa? Badala yake, wanazuoni wenzangu ambao sidhani kama tunazo facts za kutosha tunaendelea kumshutumu Lowassa na kumwona kama vile ni corrupt na kiongozi asiyefaa. It is not fair.
Mimi simlaumu Lowassa kujitoa CCM. Ni haki yake na kajieleza vipasavyo kuhusu maamuzi yake. Je, ni uamuzi wa uroho kuhusu Urais? Jamani, wanazuoni, hivi kweli tumefikia hatua ya kumwona mtu ana uroho wa Urais? Ili awe au afanye nini ambacho sisi tufunge macho, na siyo tu kutoona, bali pia kuto chukua hatua? Ikifikia hapo, basi hatuna Taifa tena!!
Taifa letu limebahatika kufika hapa lilipofika mwaka huu. Wengi hatukutarajia kwamba yale ambayo tumekuwa tukitafakari na hata kusali ghafla yameibuka. Sidhani na siamini kwamba ramani ya siasa ya Jamhuri yetu itabaki ilivyo ifikapo Desemba 2015. Ni ishara ya kheri na mwelekeo mwafaka kwa demokrasia ya Taifa letu.Naamini kwa dhati kabisa kwamba Edward Lowassa atakuwa kiongozi ambaye atasaidia ramani hii kuwba na muono mpya.
Juma Volter Mwapachu

SUPER MODEL MBONGO MAYA MIA ANAYEKIMBIZA MALASYIA NZIMA SASA HIVI ONA HAPA MWENYEWE LIVE!!

$
0
0
Super Model Maya Mia ni balahaaaaa U know halafu hapa yupo live!!









HATAMA YA MNYIKA BAADA YA LOWASA KUJIUNGA NA CHADEMA HII HAPA LIVE!!

$
0
0

 

Ikiwa ni siku Chache tangu lowassa ajiunge na chama cha chadema kumekuwepo uvumi kuwa MBUNGE wa Ubungo, John Mnyika, amekiama chama chake kutokana na chama hicho kumkalibisha Lowassa na kumpa nafasi ya juu kabisa
Ukweli wa madai haya umethibitishwa leo hii baada ya Mnyika kuhudhulia katika mkutano wa kamati kuu (CC) ya chama cha demokrasia na maendeleo
Licha ya Lissu kutoa taarifa kuwa hakuna hali ya sitofahamu ndani ya chama icho ila bado watu wamekuwa wakivumisha mambo kuwa chama icho kimevurugika baada ya wanachama kutounga ujio wa aliyekuwa waziri mkuu Edward Lowassa
Taarifa kutoka ndani ya kikao cha CC kinachofanyika katika hoteli ya Bahari Beach zilizotufikia dawati la habari clansmedia zinasema, Mnyika amehudhuria mkutano huo na kueleza kuwa kutoonekana kwake, kumetokana na matatizo ya kifamilia.
Mwanasheria mkuu wa Chadema, Tundu Lissu amethibitisha Mnyika kuhudhuria mkutano huo.
“Mnyika yupo ndani ya ukumbi wa mkutano. Anashiriki kikao cha kamati kuu. Waliokuwa wanadhani chama chetu kimepata mpasuko kutokana na ujio wa Lowassa, walikuwa wanajidanganya.” alisema Lissu
Lissu amesema, ndani ya Chadema wako wamoja, yote yaliyotokea yalikuwa mapambano yanayotokana na ukomavu wa kidemokrasia uliyopo Endelea kutufatilia kwa kila habari inayofika juu ya dawati letu la clansmedia..

LE SUPER MBEBEZZZ MUKAREEZZ KULIKO WOTE KIJITONYAMA ASHINDA KURA ZA MAONI RUKWA VITI MAALUM VIJANA LIVE!!

$
0
0
Jakcy Mzindakaya baada ya kushinda kura za maoni Viti Maalum Vijana Mkoa wa Rukwa live!!

MATOKEO ZAIDI YA KURA ZA MAONI MTOTO WA SOKOINE AFUNIKA JIMBO LA LOWASSA ONA HAPA LIVE!!

$
0
0
  Namelock Sokoine. 
Namelock Sokoine.  
By Waandishi Wetu, Mwananchi
Arusha. Binti wa Waziri mkuu wa zamani, Edward Sokoine, Namelock Sokoine ameshinda kura za maoni kugombea ubunge Jimbo la Monduli kupitia CCM huku mkwe wa Lowassa, Siyoi Sumari akishindwa Jimbo la Arumeru Mashariki.
Namelock ambaye ni mbunge wa Viti Maalumu (CCM) alipata kura 29,582 akifuatiliwa na Loota Sanare aliyepata kura 8,809 na nafasi ya tatu, ilichukuliwa na Lolinyu Mkoosu aliyepata kura 235 na Payani Leyani akipata kura 226.
Arumeru Mashariki: Sumari aliyewania jimbo hilo kwa mara ya kwanza baada kifo cha baba yake Jeremia Sumari na kushindwa na Joshua Nassari wa Chadema alipata kura kura 3,664 dhidi ya 12,071 za John Pallangyo. Mshindi wa tatu alikuwa ni William Sarakikya ambaye alipata kura 3,552 na wagombea hao waliwaacha mbali wapinzani wao wengine wanne.
Arusha Mjini: Katika Jimbo la Arusha Mjini, mfanyabiashara Philemon Mollel ameshinda kwa kura 5,320, akifuatiliwa na mfanyabiashara mwingine Justine Nyari aliyepata kura 1,894 na nafasi ya tatu, ilichukuliwa na Moses Mwizarubi aliyepata kura 1,205.
Karatu: Dk Willibrod Lorry alishinda baada ya kupata kura 17,711, Rajabu Malewa (911), John Dado (745) na Joshua Mwambo (67).
Masele ambwaga Mlingwa
Naibu Waziri, Ofisi ya Makamu wa Rais (Mazingira),  Steven Masele amembwaga waziri mwingine wa zamani, Dk Charles Mlingwa baada ya kupata 70,900 dhidi ya 669 za mpinzani wake. Wagombea wengine Abdallah Seni alipata kura 391, Erasto Kwilasa (232), Hassan Athuman (164), Mussa Ngangala (116), Hatibu Malimi (69), Wille Mzava (65) na Tara Omari (43).
Ushetu: Elias Kwandikwa (11,554) Isaya Sino (5,241) na Elfaidi Sikuli (2,007).
Kahama Mjini: Jumanne Kishimba (9,754), Kintoki Godwin (433), Nkuba Charles (389), Bundala Maiko (284), Sazia Robert (257), Kapela Robert (135), Ngalawa Adamu (126), Luhende Jerard (106), Malele Charles (91), Tunge John kura (78), Mpangama Deogratias (57), Machunda Eliakimu (56), Masanja Andrew (48) na Kambarage Masusu (28).
Msalala: Ezekiel Maige (11,575), Emmanuel Kipole (1,197), John Sukili (962), Nicholas Mabula (668), Maganza Mashala (597), John Lufunga (29) na Wankia Welema (14).
Solwa:  Mbali ya matokeo ya kata moja ambayo imerudia uchaguzi, Ahamed Salum alikuwa akiongoza kwa kura 17,485 akifuatiwa na Amos Mshandete (2,028), Cyprian Mhoja (1,586), Luhende Richard (1,273), Kasile Paul (637), Gabriel Shija (361), Renatus Chokala (357) na Hosea Somi (255).
Kishapu: Kabla ya matokeo ya kata tatu, Suleiman Nchambi alikuwa akiongoza kwa kura 13,443, William Bonda (6,143), Kishiwa Kapale (500), Limbe Moris (393), Heke Bulugu (356) na Timoth Ndanya (193).
Mawaziri watamba Kanda ya Ziwa
Waziri wa Maendeleo ya Mifugo na Uvuvi, Dk Titus Kamani ameshinda kura za maoni Jimbo la Busega baada ya kupata kura 10,697 dhidi ya mbunge wa zamani wa jimbo hilo, Dk Rafael Chegeni aliyepata kura 9,661. Buchosa: Naibu Waziri wa Uchukuzi, Dk Charles Tizeba ameibuka mshindi kwa kupata kura 26,368 dhidi ya Eston Majaliwa aliyepata 9,213.
Misungwi: Naibu Waziri wa Nishati na Madini, Charles Kitwanga ameibuka mshindi kwa kura 26,171, akimwangusha Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM, Jacob Shibiliti aliyepata kura 7,009. Shomari Chalamila alipata kura 1,840, Dk Makene Doshi (1,339), Cleophace Jerome (1,051).
Ilemela: Mkuu wa Wilaya ya Iringa Angelina Mabula ameibuka mshindi katika Jimbo la Ilemela kwa kupata kura 6,324 mbele ya Barnabas Mathayo (3,562), John Buyamba (1,167) na wagombea wengine 16.
Tabora Kaskazini: Almasi Maige (9,466), Shaffin Sumari (6,392) na Joseph Kidawa (5,965).
Bariadi: Andrew Chenge (20,200), Masanja Kadogosa (2,986) na Cosmas Manula (270).
Meatu: Salum Mbuzi (13,180), Oscar Maduhu (2,988), Romano Thomas (358) na Donard Jinasa (350).
Itilima: Njallu Daudi (44,486), Simon Ngagani (2,759) na Danhi Makanga (814).

BREAKIN NEWZZZ!!:- HATIMAYE KIMEELEWEKA JERRY SILAA NDIYE MSHINDI WA KURA ZA MAONI UBUNGE WA UKONGA LIVE!!

$
0
0

MATOKEO:- JIMBO LA UKONGA LIVE!!

1. Jerry Silaa - Kura - 10,000

2. Ramesh Patel - Kura - 7,576

DIAMOND ASITUKIA HELA ZA LOWASA ONA HAPA LIVE!!


KIJANA ALIYERUSHA MATUSI KUHUSU POLISI WALIOULIWA SITAKISHARI SASA YUPO RUMANDE ANASUBIRI KUFUNGWA ONA HAPA LIVE!!

$
0
0
Bruno Coleman Kimaryo, alikuwa akijiita majina mengi ya bandia na kutukana sana kwenye mitandao ya kijamii hatimaye safari ameingia mwenyewe choo cha kike na kunaswa na Serikali, haya ni baadhi ya majina ya bandia aliyokuwa akiyatumia kurushia maneno ya chooni huko facebook:- Bruno KIMS.....aka Wegesa Ole Sugutu.

UKITAKA KUJUA UTAMU WA UJI SHARTI UTINGISHE BAKULI ETI ONA HAPA LIVE!!

WAZIRI WA CCM ALIYEPIGWA CHINI KURA ZA MAONI AKITOA MACHOZI BAADA YA KUKATWA NA WANANCHI LIVE!!

MKUU WA WILAYA YA KINONDONI MH. MAKONDA NYOTA INAZIDI KUWAKA TATIZO NI NYOTA U KNOW LIVE!!

KATI YA LOWASA NA DR. SLAA CHADEMA WAMCHAGUA LOWASA NA KUMPUMZISHA KATIBU WAO MKUU SLAA ONA HAPA LIVE!!

$
0
0


Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe (kulia) akiwa na Katibu wake, Wiibrod Slaa
Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe (kulia) akiwa na Katibu wake, Wiibrod Slaa

Chadema ‘wampumzisha’ Dk. Slaa



CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), kimempumzisha Katibu Mkuu wake Dk. Wilbroad Slaa. Anaandika Sarafina Lidwino … (endelea).
Aidha, wanachama wake wametakiwa kuacha kuwa hofu kutokana na ujio wa Lowassa kwa kuogopa kunyanganywa vyeo vyao na wafuasi wake.
Mbowe amesema, “inawezekana Slaa naye anahofu juu ya ujio wa Lowassa kama ilivyo kwa wanachama wengine, wakidhani kuwa nafasi zao zitachukuliwa na wananchama wapya”. Hayo yanabainishwa leo Mwenyekiti wa Taifa wa Chama hicho Freeman Mbowe alipokuwa alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari.
“Katika hatua zote hizo tulikuwa sambamba na Slaa lakini baadae alibadilika ghafla na kutofautiana na Kamati kuu.Na mimi mwenyewe binafsi jana nimekaa nae zaidi ya masaa mawili nikijaribu kuongea nae lakini hatukufikia muafaka” amesema Mbowe.
Amesema maamuzi hayo ya kumpumzisha Slaa yameamuliwa na Kamati kuu ya Chadema baada ya kuwa katika mazungumzo ya muda mrefu bila kupata muafaka wa hatima ya ukimya wake.
Akizungumza na waandishi kabla ya kuanza Mkutano wa Baraza Kuu Chadema Mbowe amesisitiza kuwa Slaa alibadilika ghafla baada ya Kikao Cha Kamati Kuu. Mbowe ameeleza kuwa, awali Chama kilikaa vikao vingi kujadili juu ya ujio wa Waziri mstaafu Edward Lowassa kujiunga na Chadema na kufikia makubaliano yaliyowahusisha viongozi wote wa Chama akiwemo Slaa.

Mbowe amesema, chama hakiwezi kusimama kufaya shughuli zake kikisubiri maamuzi ya mtu mmoja hivyo kitaendelea na kazi zake hususani katika kipindi hiki kigumu cha uchaguzi.
Mbali na hilo, amesema, “Chama kipo tayari kumpokea wakati wowote atakapokuwa tayari kurudi katika nafasi yake na sisi bado tunampenda na kumheshimu kama kiongozi”
“Leo nimeamua kuweka wazi suala hili baada ya kusikia na kuona vyombo vya habari mbalimbali vikiripoti habari zisizo za kweli ya kwamba Slaa amejiuzu na kwamba Chama kimempora mali zake na kumtishia habari hizo sizakweli na wala chama hakina ugomvi nae”.
Amesema, wanachama hawatakiwi kuhofia chochote juu ya ujio wa Lowassa na wafuasi wake kwani Chadema ni chama cha wananchi kwa yoyote atakae hitaji kujiunga anakaribishwa.
“Lakini hofu hii haipo kwetu tu ipo hata kwao Chama cha mapinduzi (CCM) kwani hawajawahi kupata hofu na viboko kama hivi vya kuondokewa na wafuasi wengi tena kwa wakati mmoja kama mwaka huu”.
Amesema CCM hadi sasa bado hawajielewi kutokana na mapigo mengi yaliyowapata kutokana na kuondokewa na kada wao mkubwa, na wengine bado wanakuja na hii ndio furaha ya chadema ili kuweza kuimaliza CCM Oktoba Mwaka huu.“Ni lazma tuitumie fursa hii tuliyoipata na hatuwezi kuiacha. Lengo letu ni kuwa na wafuasi wengi zaidi haswa kutoka CCM ili tuzidi kuwamaliza kabisa tumeshawapokea wengi na tutazidi kuwapata wengi zaidi”.

Akizungumzia mkutano mkuu utakaofanyika kesho katika ukumbi wa Mlimani city Dar, ambapo amesema utamtangaza rasmi mgombea urais kwa tiketi ya Chadema pamoja na kumtangaza mgombea mwenza wa chama hicho.

KUHUSU DR. SLAA HABARI KAMILI HII HAPA LIVE!!

$
0
0
Iddy Harnaa Mkwama's photo.




¤Hii picha ilipigwa Jumapili ya tarehe 26-Jul-2015 Bahari Beach Hotel ¤Ndio siku ya mwisho ambayo Dr Slaa alionekana kwenye vikao vya CHADEMA ¤Alitoa masharti ya jinsi ya kumpokea Lowassa, masharti ambayo yalipuuzwa.

 

¤Kesho yake (Jumatatu 27-Jul-2015) akaona press conference ambayo James Mbatia alipewa kazi ya kumkaribisha EL UKAWA
¤Alichofanya Dr Slaa ni kuandika barua ya kujiuzulu ukatibu mkuu. Baadaye akaandika barua ya kujivua uanachama wa CHADEMA. Siku nyingine akakabidhi gari alilokuwa analitumia kama katibu. Ijumaa iliyopita (31-Jul-2015) alikabidhi nyaraka zote za chama alizokuwa nazo.
 

¤Hivi sasa hakuna kiongozi hata mmoja wa CHADEMA mwenye uwezo wa kuwasiliana naye. Simu yake haipatikani.
¤Inasemekana ana mpango wa kuachana kabisa na siasa.
¤Moja ya maandalizi yaliyofanyika ni Tundu Lissu kusema yeye ndio aliandika "List of Shame" na Dr Slaa aliisoma tu. Mwaka 2007 Lissu hakuwa hata mbunge.
 

¤Mbowe anasema Dr Slaa amepewa likizo. Umewahi wapi kuona mwanajeshi anachukua likizo kipindi ambacho vita inakaribia kuanza? ¤Kimkakati, nafasi yake imetangazwa kuwa wazi labda hadi uchaguzi upite ili isiathiri matokeo ya uchaguzi.

SOMETIMES MASUDI KIPANYA ANAFURAHISHA SANA ONA KATUNI YA LEO NI NOMAAA U KNOW LIVE!!


SUPER STAR ACTRESS IRENE UWOYA ASHINDA KURA ZA MAONI TABORA UVCCM ONA HAPA LIVE!!

$
0
0
MATOKEO UVCCM VITI MAALUM TABORA:- 1. Irene Uwoya - Kura - 34 2. Mariam Shamte - Kura 3 3. Zahra Michuzi - Kura 2




AVEC AWILO LONGOMBA KATU KATUUUU COMA DANCE!! ZIPOMPA POMPA LE LUCIANA DEMINGONGO LIVE MUSIC VIDEO!!

MKUU WA WILAYA YA KINONDONI MH. MAKODA SASA NI MOTO WA KUOTEA MBALI SANA ONA HAPA LIVE!!

$
0
0

"Leo tumezindua Jogging Club ya Mburahati, pia tumezindua ofisi pamoja na Miradi midogo midogo, na kuwakabidhi mashine ya Max malipo yenye thamani ya shilingi milioni moja na laki tano.
Nimatumaini yangu vijana wote tutawajibika ili tujikwamue kiuchumi. Hakuna atakaetusaidia kama hatujachukua hatua sisi wenyewe."

LE SUPER MBEBEZZZ MUKAREEZZ KULIKO WOTE ASHINDA KURA ZA MAONI KAGERA VITI MAALUM VIJANA LIVE!!

$
0
0
Khalima Bulembo baada ya kushinda kura za maoni Viti Maalum Vijana Mkoa wa Rukwa live!!

EDWARD LOWASA KUTIMUA VUMBI MAPEMA KESHO.

Viewing all 32622 articles
Browse latest View live


<script src="https://jsc.adskeeper.com/r/s/rssing.com.1596347.js" async> </script>