↧
SIKIYA THE ONLY SONG ILIYOWAHI KUTUNGWA NA DRUMMER BOY WA ORCH. LIPUA LIPUA AVEC NSAYI NONO NKUKA "Nsayi" LIVE!!
↧
LE MUTUZ NATION LIVE AT MY OFFICE DOWNTOWN TANCOT HOUSE 2ND FLOOR MWANAUME NI KAZI KWANZA LIVE!!
↧
↧
"Yanini" WIMBO MMOJA TU ULIOPIGWA NA VERKYS KIAMUNGANA MATETA WAZELA MBONGO WA VEVE STAR & MOMBASA VATA JUJUMAN WA LIPUA LIPUA LIVE!!
↧
AJALI YAUA NDUGU WATANO WALIKUWA WANATOKA KUZIKA
Ajali iliyotokea jana katika kijiji cha Mavuji wilayani Kilwa imesababisha vifo vya watu watano wa familia moja ambapo walikuwa wanatoka kuwazika ndugu zao wawili juzi mjini Lindi baada ya marehamu hao kupata ajali.
Waliofariki katika ajali hiyo ni pamoja na Bi Saida ambaye ni mama Mzazi wa Marehemu, Shiraz Jack Magongo aliezikwa Juzi, Shirin Jack Magongo ambae ni Mama Mzazi wa Marehemu Samia (MRS Lupanda) pamoja na Marehemu Shiraz.
Marehemu Mwingine ni Ajira Shiraz Jack Magongo Nargis ambaye ni dada yao wa mama mkubwa na Mdogo ambaye kwa waliokuwa Lindi ndiye mmiliki wa nyumba ya Gift Guest na walio Dar yupo Livingstone Str maarufu kwa uuzaji wa chumvi, pamoja na Meja Hussein Bhatia ambae ndie alikuwa dereva wa gari hilo ambaye alifariki baadaye.
Maiti ya marehemu Bi Saida, Shirin na Nargis zinatarajia kuzikwa Dar huku maiti ya Marehemu Meja Hussein Bhatia na Ajira Shiraz ikiwatarajiwa nayo kuzikwa mkoani Lindi.
Katika ajali hiyo dada mkubwa wa marehemu Shiraz na Shirin, Yasmin Jack Magongo walikimbizwa katika hospitali jijini Dar es Salaam kwa matibabu.
Mwingine ambaye ni Salma Mohamed Zaid, mtoto wa Mama Malaika Hotel (mama mzazi wa marehemu Ajira Shiraz aliyefariki katika ajali hiyo) ametoka salama katika ajali hiyo.
Chanzo cha ajali hiyo kimeelezwa kuwa ni kutanda kwa moshi barabarani na gari aina ya Noah T594 DDH lililosababisha watu hao kufariki dunia kuligonga basi la SB lililokuwa limesimama kando ya barabara.
↧
BREAKING NEWZZ..!, BAADA YA KUPIGWA STOP CHADEMA... DR. SLAA AFUNGUKA, SOMA HAPA ALICHOSEMA

Siku tatu baada ya Baraza Kuu la Chadema kuridhia kumpumzisha kwa muda Katibu Mkuu wa chama hicho, Dk Willibrod Slaa baada ya kutofautiana na Kamati Kuu kwa kumkaribisha waziri mkuu wa zamani, Edward Lowassa, kiongozi huyo amesema yupo salama na wakati mwafaka ukifika atazungumza ya moyoni.
Akizungumza kwa mara ya kwanza na gazeti la Mwananchi tangu Chadema imkaribishe Lowassa na hatimaye kumpitisha kuwania urais kupitia muungano wa Ukawa, Dk Slaa amesema amekuwa akisikia mengi yakisemwa juu yake lakini yote yamekuwa yakimchekesha tu.
Hakuhudhuria vikao muhimu vya chama hicho na vile vya Ukawa, vikiwamo; wakati Lowassa akitambulishwa rasmi, akichukua fomu, kikao cha Baraza Kuu na juzi Mkutano Mkuu na hakuwa akipatikana kwa simu yake ya mkononi.
Wakati kimya kikitawala juu ya hatima yake, baadhi ya vyombo vya habari vimekuwa vikiandika kuwa amejivua uanachama Chadema.
Lakini jana alisema: “Naangalia mambo mengi yanayoendelea kwenye mitandao halafu ninacheka tu, usifikiri sifuatilii, nafuatilia kinachoendelea na ninabaki nikicheka.”
Kuhusu hatima yake kisiasa na madai ya kujiuzulu uanachama ndani ya Chadema, alisema hawezi kuzungumza lolote kwa sasa na atafanya hivyo wakati mwafaka ukifika.
“Usijali wakati wangu wa kuzungumza ukifika nitasema tu, sasa hivi nawaachia mzungumze, lakini nitazungumza,” alisema.
Kadhalika, alipoulizwa kuhusu taarifa zilizozagaa kuwa maisha yake yapo hatarini kwa kuwa anatishwa, Dk Slaa alisema hata hilo pia atalizungumzia wakati mwafaka ukifika.
“Ndiyo hayohayo ninayosema, wala msijali nitazungumza wakati ukifika,” alisema na kusisitiza: “Nipo salama.”
Dk Slaa alisema kwa sasa yupo mapumzikoni nje ya jiji la Dar es Salaam ingawa hakutaka kueleza ni eneo gani.
Juzi, Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe alifafanua tofauti iliyojitokeza kati ya Kamati Kuu ya Chadema na Dk Slaa wakati wa mchakato wa kumpokea Lowassa.
Katika mkutano huo wa Baraza Kuu la Chadema, Mbowe alisema wamekubaliana katibu mkuu huyo apumzike kwa muda... “Nina hakika kwa tabia na hulka za Dk Slaa… kwa sababu anajua tunampenda na yeye anakipenda chama hiki, tunamwombea kwa Mungu ampe nguvu na ujasiri wa kuona kwamba kauli ya wengi ni kauli ya Mungu.”
Ndesamburo na siri nzito
Mbunge wa Moshi Mjini, Philemon Ndesamburo na makada wengine wa Chadema, jana walikwenda kuonana na Dk Slaa nyumbani kwake na kufanya naye kikao cha faragha.
Picha zilizomuonyesha Ndesamburo akiwa na Dk Slaa na makada wengine akiwamo Mjumbe wa Kamati Kuu ya Chadema, Jaffar Michael, zilisambaa kwa kasi katika mitandao ya kijamii jana na kuibua mijadala.
Baadhi ya waliochangia mijadala hiyo walidokeza kuwa huenda Ndesamburo anayeheshimika ndani ya chama hicho alikwenda kujaribu kusawazisha hali ya mambo.
Mkuu wa Idara ya Habari wa Chadema, Tumaini Makene alikiri kuwa picha hizo ni halisi, baadhi zilipigwa juzi na nyingine jana mchana, lakini hakutaka kuingia undani wa mkutano wa wanasiasa hao.
Ndesamburo alithibitisha kukutana na Dk Slaa: “Ni kweli tulikwenda, kwani kuna tatizo gani? Si mzee mwenzangu? Halafu bado ni mwanachama wetu, hajatoka Chadema, hivyo tuna kila haki ya kwenda kumsalimia.”
Alipoulizwa kama alikwenda kumsihi Dk Slaa arejee kuendesha mapambano ya kuing’oa CCM, Ndesamburo alisisitiza kuwa walikwenda kumsalimia.
Michael alipoulizwa nia ya safari hiyo alijibu kwa kuuliza; “Dk Slaa ni katibu mkuu wetu kwani tunazuiwa kwenda kumsalimia?”
Dk Slaa aligombea urais mwaka 2010 na kushika nafasi ya pili baada ya Rais Jakaya Kikwete na ndiye aliyekuwa akitajwa kuwania tena nafasi hiyo kupitia Chadema na Ukawa kabla ya “kubadili gia angani” na kumteua Lowassa.
↧
↧
RAIS JAKAYA KIKWETE NA MH MAGUFULI WAJIPIGA SELF ZAKUTOSHA.
↧
TAFAKARI YA KIPANYA NAIBU WAZIRI ALIYEHAMA CHAMA.
↧
MH CHENGE AFUNGUKA MAKUBWA KUHUSU VIJISENTI VYA ESCROW.
↧
DIAMOND PLATNUM AJISIFIA MBELE YA RAIS KIKWETE.
↧
↧
KIGWANGWALA KAM-BEZA LOWASSA MTANDAONI, JIONEE HAPA
↧
WAANDISHI WA MITANDAO YA KIJAMII WAPEWA ELIMU YA AFYA YA UZAZI






BAADHI ya wanahabari wa mitandao ya jamii jijini Dar es Salaam wamepewa mafunzo juu ya taarifa za uzazi na afya ya mama na mtoto ili waweze kuelimisha zaidi jamii kupitia mitandao yao dhidi ya taarifa hizo. Akizungumza wakati akifungua semina hiyo, Mkurugenzi wa Taasisi ya Kupunguza Matatizo ya Mapafu Duniani iliyopo nchini Tanzania (WLF), Dk. Nguke Mwakatundu alisema taasisi yake imeamua kutoa mafunzo hayo kwa wanahabari hao ili waweze kuwa mabalozi wazuri wa kuelimisha jamii kupitia mitandao yao juu ya umuhimu wa kupambana na vifo vya mama na mtoto vinavyoendelea kutokea kila uchao. Alisema kazi ya kupunguza vifo vya mama na mtoto si jukumu la madaktari au hospitali pekee lakini jukumu la jamii nzima kukabiliana na huduma hiyo, alisema vyombo vya habari ikiwemo mitandao ya jamii inakilasababu za kuonesha mapungufu na kueleza changamoto katika huduma za afya zinazotolewa kwa lengo la kuboresha zaidi huduma hizo. Alisema tatizo la elimu ya afya ya uzazi ni kubwa nchini kwani takwimu zinaonesha kwa kila saa moja kuna mama anayepoteza maisha kutokana na matatizo ya uzaziSerikali. "...Kila siku kuna akinamama takribani 24 wanapoteza maisha kutokana na matatizo ya uzazi nchini," alisema Dk. Mwakatundu. Awali akizungumzia hali halisi ya uzazi wa mpango nchi, Meneja Mawasiliano wa WLF, Victoria Marijani alisema kuna faida kuwa ya kuzingatia Uzazi wa Mpango kwani ni uwekezaji wenye faida na endelevu ambao unachangia kupunguza vifo vitokanavyo na uzazi kwa kiasi kikubwa hadi asilimia 44. Aliongeza kuwa uwekezaji huo wa ziada katika afya, elimu, usawa wa kijinsia na uwepo wa sera wezeshi za kiuchumi vitaiwezesha nchi kupata manufaa yatokanayo na ukuaji wa haraka wa uchumi. Alisema familia zinazotumia uzazi wa mpango zinakuwa na uwezo wa kuwatimizia watoto mahitaji yao muhimu kama chakula, elimu, mavazi, huduma za afya na makazi. "...Atapata muda wa kushiriki katika shughuli za jamii, Atamudu kujiwekea akiba, Atakuwa na amani na upendo kwa familia yake. Alisema kiwango kikubwa cha vifo vya watoto chini ya miaka 5 (vifo 81 kwa vizazi hai 1000) Kiwango kidogo cha utumiaji wa njia za kisasa za uzazi wa mpango (Asilimia 27). Wastani wa utumiaji wa njia za kisasa za uzazi wa mpango hapa nchini bado ni mdogo. Ni asilimia 27 tu ya wanawake walio kwenye umri wa kuzaa ndio wanaotumia njia za kisasa za Uzazi wa Mpango. *Imeandaliwa na www.thehabari.com
↧
MAGUFULI ALIVYOWASILI MLIMANI CITY
Mgombea wa Urais kupitia CCM Dk. John Pombe Magufuli akiwasili kwenye ukumbi wa Mlimani City tayari kuhudhuria hafla maalum ya kumshukuru na kumuaga Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete ,Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, pamoja na kumpongeza na kumkaribisha Mheshimiwa John Pombe Magufuli.wengine pichani ni Ruge Mutahaba ,Katibu wa Itikadi na Uenezi CCM Taifa Nape Nnauye .
Mgombea wa Urais kupitia CCM Dk.John Pombe Magufuli akisalimiana na Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni Mhe.Paul Makonda.
Mgombea wa Urais kupitia CCM Dk.John Pombe Magufuli akisaini kitabu cha wageni
Mgombea wa Urais kupitia CCM Dk.John Pombe Magufuli akisalimina na Mbunge wa Jimbo la Bumbuli na Naibu Waziri wa Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia, Mhe. January Makamba
Mgombea wa Urais kupitia CCM Dk.John Pombe Magufuli akiwa kwenye picha ya pamoja na msanii Diamond ,Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana ,Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi Nape Nnauye na Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni Mhe. Paul Makonda na Mbunge wa Jimbo la Bumbuli na Naibu Waziri wa Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia, Mhe. January Makamba.
↧
DIAMOND PLATNUM AMPAKULIA CHAKULA ALI KIBA.
↧
↧
WEMA SEPETU AJIWEKA KARIBU NA MH MAGUFULI.
↧
EDWARD LOWASA AFUNGUKA KUHUSU WASANII YALIOJIRI JANA.
Nimeambiwa leo Rais na Magufuli watakuwa na dinner na kundi la vijana wasanii. Wasanii hawahitaji dinner, wanahitaji hakimiliki ziboreshwe
Dinner ya kweli kwa hawa vijana ni hakimiliki kwa kazi zao, si dinner ya namna hii. Huu ni ulaghai. Wasanii amkeni
↧
BILIONE AFANYA KUFURU.
↧
MSANII WA BONGO FLEVA AIBUKA MSHINDI KURA ZA MAONI.
↧
↧
MBUNIFU WA MITINDO AMINA PLUMMER ATOA MADA NAMNA KUJITAMBUA KWENYE SEMINA YA KUWAWEZESHA WANAWAKE WAJASIRIAMALI INAYOANDALIWA NA MANJANO FOUNDATION

Mbunifu na Mmiliki wa Maduka ya Amina Design Ambaye pia ni Mentor wa Taasisi ya Manjano Foundation Amina Plummer Akitoa Mada kwenye Semina ya Kuwawezesha Wanawake Kuwa Wajasiriamali kupitia Vipodoz Vya Luv Touch Manjano Iliyoandaliwa na Manjano Foundation Kwa Lengo la Kuwajengea Udhubutu Wanawake Kufanya biashara pia namna ya Kujiwekea Akiba na Kutumiza Malengo yao. Taasisi ya Manjano Foundation, ambayo imeanzisha jukwaa kwa ajili ya kuandaa Miradi ambayo itamuinua mwanamke wa Kitanzania kwa kumwondolea umasikini wa kipato na ambayo itakuwa ni chachu ya kubadili yale yote yaliyoyazunguka maisha yake. Taasisi hii limekwishazindua mradi wenye kubeba bendera yake, Manjano Dream-Makers, mradi unaokusudia kuzaa kizazi kipya cha wajasiriamali wanawake kwa kutumia kipodozi cha LuvTouch Manjano tu
Afisa Mtendaji Mkuu wa Shear illusions Ltd Mama Shekhar Nasser (Katikati) Akiwa na Mbunifu Amina Plummer (Kushoto ) Pamoja Afisa Mtendaji Mkuu wa Women an Youth Empowerment Program Kutoka Uganda Dada Remmie Male.
Mbunifu na Mmiliki wa maduka ya Amina Design Amina Plummer ni mmoja kati ya Mentors 15 watakao wapa muongozo washiriki 30 wa mradi wa Manjano Foundation. Amina aliwapa somo la kujifahamu kama wajasiriamali chipukizi kuwa wasilimbuke pale ambapo mafanikio yanapo anza kuja. Aliwaeleza kuhusu umuhimu wa kujiamini, kumuamini Mungu, kuwakarimu wateja, kuweka akiba Akiwa Sambamba na Afisa Mtendaji Mkuu wa Women an Youth Empowerment Program Kutoka Uganda Dada Remmie Male
Mbunifu Amina Plummer ni mmoja katika Picha ya Pamoja na Baadhi ya washiriki wa Semina hiyo inayoandaliwa na Taasisi ya Manjano Kupitia Bidhaa za Luv Touch Manjano.
Afisa Mtendaji Mkuu wa Shear illusions Ltd Mama Shekhar Nasser na Mbunifu Amina Plummer Pamoja Afisa Mtendaji Mkuu wa Women an Youth Empowerment Program Kutoka Uganda Dada Remmie Male. Katika Picha ya Pamooja na Washiriki wa Semina hiyo..
↧
DIAMOND KAIBIWA MTOTO SIO WAKE KISA KIMO HUMU DUH HIVI HII SURA ITAKUWA YA DIAMOND KWELI?
↧
THE MAGAZETI YA BONGO LEO FRIDAY /IJUMAA 7/8/2015 LIVE!!
↧